2013-11-11 15:48:01

Kifo kiko nyuma yetu,na mbele yetu kuna Mungu wa walio hai- Papa


Baba Mtakatifu Francisko, kabla ya kusali sala ya Malaika wa Bwana, mbele ya mahujaji na wageni waliokusanyika katika Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, Vatican, alitoa hotuba fupi, akilenga zaidi somo la Injili la Jumapili , ambapo Yesu alikabiliana na Masadukayo , ambao hawakusadiki juu ya ufufuko wa wafu.

Francisko alisema,Masadukayo waliitoa swali hili la mwanamke kuolewa na ndugu saba , kwa makusudi ya kumtega na kukejeri ufahamu wa Yesu juu ya Imani katika ufufuo. Masadukayo walihoji sasa mke huyo aliyeolewa na wamanume saba, ambao walikufa mmoja baada ya mwingine, je wakati wa ufufuo , nani atakuwa mme wa mwanamke huyo ?
Awali ya yote, Papa alisema , Yesu anaeleza kwamba maisha baada ya kifo ni maisha mengine tofauti na maisha yetu ya duniani. Uzima wa milele ni maisha tofauti, yenye mwelekeo tofauti ambapo , miongoni mwa mambo mengine, hapatakuwepo tena maisha ya ndoa. Kufufuka, Yesu anasema, ni kuwa mwili mwingine kama malaika , na wao wataishi katika hali mbalimbali, ambazo sisi hapa duniani hatuwezi kuziishi wala hatuna sura yake inavyo fanana hatunayo hata kimwazo tu.

Lakini basi, Papa Francisko aliendelea , Yesu anatoa majibu na kuzungumzia suala hili, na kutoa mfano wa tukio la Musa na kijiti cha moto, ambapo Mungu alijifunua mwenyewe kuwa ni Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo. Jina la Mungu , Papa Francis alielezea, linatufugamanisha na majina ya wanaume na wanawake ambao Yeye ana mahusiano nao. Ni kiungo chenye nguvu, kuliko kifo. Hii ndiyo sababu Yesu anasema kwa uthabiti kwamba, Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai kwa wote walioitwa kuishi kwake (Luka 20:38 ). Yesu ndiye kiungo muhimu,Yeye aliye Uzima na Ufufuo , kwa sababu kwa upendo wake alikubali kusulubiwa na kukishinda kifo .

Katika Yesu , Papa alisema, Mungu anatupa uzima wa milele : Yeye anautoa kwa kila mtu. Shukrani kwakeYeye anayetupa tumaini hili, maisha tumaini lililo kuu kuliko yote. Maisha ambayo Mungu ametuhifadhia ghalani mwake si tu kwa ajili ya maisha bora zaidi lakini ni imaisha ambayo akili yetu ya kibinadamu, haiwezi kufikia upeo wake, kwa sababu Mungu daima , hutushangaza kwa upendo na huruma yake.

Kwa hiyo, Francis Papa alielezea, kitakachotokea ni kinyume kabisa na kile Masadukayo walivyotarajia. Maisha ya hapa duiniani hayawezi kuwa kiwango cha maisha ya milele : ni umilele, ulio kinyume na maisha yetu , ni umilele wenye kuangazia maisha ya hapa duniani na kutoa tumaini kwetu. Iwapo tutatazama kwa macho ya kibinadamu , Papa aliendelea , tunakuwa na mwelekeo wa kuona kwamba, njia ya maisha tunayo itembea inaelekea katika kifo. Lakini Yesu anatutazamisha katika lengo kuu la Maisha, akituthibitishia kwamba tunatembea katika safari inayokwenda kutoka kifo kuelekea maisha kamili ya umilele.
Hivyo , Papa alihitimisha hotuba yake na maelezo kwamba kifo kiko nyuma yetu, si mbele yetu . Mbele yetu ni Mungu wa walio hai, aliyeshinda hila zote za kifo na dhambi na mauti, na kuwa mwanzo wa maisha mpya ya furaha na mwanga na usio na ukomo. Lakini tayari katika dunia hii - katika sala, katika Sakramenti , katika udugu - sisi kukutana Yesu na upendo wake, na ili tuweze kupata ladha ndogo ya maisha ya kufufuka.








All the contents on this site are copyrighted ©.