Papa Francisko kukutana na Rais Putin mjini Vatican
Rais Wladimir Putin wa Russia, tarehe 25 Novemba 2013 majira ya jioni, atakutana na
kuzungumza na Baba Mtakatifu Francisko mjini Vatican. Habari hizi zimethibitishwa
na Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican. Tukio hili la kihistoria litafanyika
mara tu baada ya Maadhimisho ya Mwaka wa Imani, uliotangazwa na kuzinduliwa na Baba
Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI. Hili nalo litakuwa ni tukio la kihistoria baina ya
viongozi hawa wawili.