MWUCE inavyokabiliana na changamoto za maboresho ya elimu nchini Tanzania
Hotuba ya Principal kwenye mahafali ya sita ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (Cha
Chuo Kikuu cha Mt. Augustino cha Tanzania) Mwenge- 02-11-2013 1 Utangulizi Mhashamu
Baba Askofu Mkuu wa Chuo, sisi wana Mwenge tunaona fahari sana kuwa nawe siku hii
ya leo katika kuadhimisha Mahafali ya Sita ya Chuo chako hiki. Karibu sana Baba Askofu.
Aidha naomba kuchukua fursa hii kukupongeza Baba Askofu kwa kuteuliwa kuwa Rais wa
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania na hivyo pia kuwa Mkuu wa Chuo cha Mtakatifu
Tanzania. Pongezi sana Baba Askofu. Huo ni wajibu mkubwa unaodai muda na majitoleo
mengi licha ya kuwa na jimbo lako mwenyewe. Tunakuhakikishia sala zetu sisi wana Mwenge
ili ujaliwe afya na nguvu ya kuendeleza wajibu hizo nyingi.
Mhashamu Baba Askofu
Mkuu wa Chuo, Chuo cha Mwenge kimesimikwa katika mtazamo kwamba elimu ni taa ya kuangaza
ili watu waweze kuona na kwa kuona waweze kupiga hatua na kusonga mbele. Mwasisi wa
chuo hiki kwa kutambua kwamba elimu ni mwanga alichagua KAULI MBIU yake kuwa ni LUX
MUNDI kwa Kiswahili MWANGA WA DUNIA ili iwe changamoto katika jitihada ya shughuli
za chuo za kila siku kumwangazia mwanadamu aweze kupiga hatua ambazo zitamletea ufanisi
katika maisha yake na yale ya jamii anayotazamia kuihudumia.
Mheshimiwa Mgeni
Rasmi Chuo kimeendelea kusimamia azma hiyo ya kumtayarisha Mtanzania mtaalamu ambaye
yuko tayari kuhudumia Watanzania wenzake kwa kutumia maarifa aliyopata kwa weledi
na kwa uadilifu.
Chuo kilianza kama chuo cha ualimu yakiwa ni matayarisho
ya kuwa chuo kikuu. Julai 2005 chuo kilipata usajili kuwa Chuo Kishiriki cha Mt. Augustino
Tanzania. Chuo kinaendelea kukua kwani programu zinazofundishwa chuoni hapa zimeendelea
kuongeza mwaka hadi mwaka. Kutoka Programu ya Ualimu wa masomo ya Sayansi iliongezwa
programu ya Ualimu wa masomo ya Sanaa kwa sasa tunazo programu 24......zinazojumlisha
programu za astashahada na shahada za uyamili. Programu hizo zimelenga katika kutoa
elimu kwa maeneo maalumu ambayo jamii ya Kitanzania yanahitaji kwa sasa. Programu
hizo zinajumlisha uhasibu, sheria, computa science, Geografina na mazingira, Sociology
and social work, Mathematics and Statiscs na Ualimu kwa ngazi za shahada ya kwanza
na shahada ya Uzamili. 2 Mahafali Mhashamu Baba Askofu, Chuo cha Mwenge leo
kinaadhimisha Mahafali ya Sita kama Chuo Kikuu Kishiriki cha Chuo Kikuu cha Mt. Augustino
Tanzania. Ni adhimisho la pekee kwa sababu kwa mara ya kwanza Chuo kinahitimsha wanachuo
waliosomea Ualimu katika ngazi ya shahada ya Uzamili...ambao idadi yao ni kumi na
moja. Jumla ya wahitimu wote ni 465....................
Hakuna shaka kwamba
siku hii ni ya pekee sana kwa wahitimu wetu. Tunawapongeza kwa juhudi waliyoiweka
hadi kufikia siku hii. Tunaposherehekea nao watambue kwamba tunamatazamio makubwa
kwao kwamba wataenda kuishi kile ambacho wamejifunza hapa Chuoni. Uhakika wana jumuiya
wa MWUCE waiona nao ni kwamba wahitimu waliotangulia wamekuwa wanafanya vema kazini
kwa kuwa wengi wao wameonesha kuzingatia mafunzo waliopata. Nanyi tunawaasa mwende
mkahudumie jamii ya Watanzania kwa kuwajali na kuweka mbele maslahi yao.
Aidha
muwapo kazini kumbekeni kwamba utaalamu daima unadai kuendelea kusoma ili kujiimarisha
katika fani na kupata maarifa mapya. Tafadhali dhana ya kwenda kwenye warsha au semina
ili kupata malipo tuachane nayo...tutazame mbele na kuona umuhimu wa kuongezea maarifa
ili uweze kufanya kazi yako vizuri zaidi. Kwa masikitiko makubwa utamaduni wa kutafuta
semina au warsha kwa ajili ya malipo umejikita sana katika jamii – kuendeleza huo
ni kuua taaluma na hata utendaji unakuwa hafifu kwani kunakuwa hakuna kujishughulisha
katika kutafuta elimu zaidi itakayoinua viwango na kuimarisha utendaji.
Muwe
mfano wa kuigwa katika kufanya kazi kwa juhudi na uelewa. Ijue fani yako na uiimarishe. 4
Mtaalamu wa Kitanzania Mheshimiwa Mgeni Rasmi, wajibu wa shule na vyuo ni kufundisha
wanafunzi ili wakue katika maarifa na ujuzi. Chuo cha Mwenge kinatambua wajibu wake
wa kukuza vipaji kwa kuwatayarisha wanachuo kuwa wataalamu mahiri katika maeneo ya
ujuzi waliyoyachagua. Utaalamu unadai uwepo wa nia thabiti ya kulijua somo kwa kulisoma
kwa bidii na kulenga kujiimarisha katika taaluma yenyewe. Wanachuo wanakumbana na
changamoto nyingi zikiwemo za kukosa uwezo wa kiuchumi na hivyo kusoma kwa shida hasa
kwa wale wasiokuwa na mikopo ya serikali, wengine wanakuwa na majukumu ya kusomesha
wadogo zao au ndugu zao wakati wenyewe wanasoma na hata wengine wanakuwa hawajatulia
na kuamua kwamba wanataka kujikita katika kusoma badala ya kuhangaika na maisha ya
mitaani na kusoma.
Chuo kinafanya jitihada kuona kwamba wanachuo wanaojidahili
kwenye Chuo cha Mwenge wanazingatia masomo na kufuata maelekezo na taratibu za Chuo
kama zilivyopangwa na uongozi wa chuo. Miongozo hiyo imewekwa ili kuhakikisha kwamba
mwanachuo anaongozwa kwa utaratibu utakaomwezesha kukabiliana na mazingira anayoenda
kufanyia kazi na pia kuwa tayari kuingia kwenye mashindano ya soko la ajira nchini
na hata nje ya nchi. Inabidi tukiri kwamba sehemu Fulani ya maandalizi ya wataalamu
wetu inakumbwa na kigugumizi – kwa mfano: Kwa sehemu kubwa mazingira ya nchi yetu
kielimu yameelekea kuweka mbele sana upatikanaji wa cheti ili kupata ajira.
Matokeo
yake kama ambavyo tumesoma kwenye vyomba vya habari karibuni vijana wengi wamejikuta
wakitafuta vyeti mitaani (fake certificates) kutafutia kazi...hata wengine wanadiriki
kutumia vyeti vya namna hiyo kuingia vyuoni. Hiyo ni dhambi ya kipindi hiki na inalingana
na dhambi ya kuibia mitihani, nakadhalika. Wanahitimu wetu muendapo kazini muwe wabunifu
na siyo watu waliokosa ujasiri wa kuthubutu. Tumewafunza namna ya kupata vitendea
kazi hata pale ambapo vitendea kazi vinapokuwa hafifu – remember to improvise.
5
Changamoto Utoaji wa elimu ya juu unadai maandalizi na uwezo mkubwa katika maeneo
mengi. Kwa sasa Tanzania imekuwa na vyuo vingi vya elimu ya juu na hili linaongeza
changamoto kwa vyuo vyenyewe. Kati ya changamoto ambazo Chuo Kikuu Ksihiriki cha Mwenge
kinakabiliana nazo ni: Upatikanaji wa wanafunzi waliofaulu vizuri
katika masomo ya kidato cha sita hasa masomo ya sayansi. Wanachuo kukosa mikopo
ya serikali na hivyo kupangwa chuoni na mwisho wanaamua kurudi nyumbani kwa kukosa
uwezo wa kujilipia Uendeshaji wa Programu za sayansi ni gharama sana. Hakuna shaka
kwamba nchi yetu inahitaji wataalamu wa sayansi na teknolojia ambao watasaidia kusukuma
maendeleo ya nchi yetu. Chuo kimeendelea kuwekea mkazo upatikanaji wa wataalamu wa
sayansi lakini matumaini yetu kwamba serikali itasaidiana na vyuo vinavyotoa elimu
hiyo haujaonekana kupata mwitikio.
Utoaji wa
Scholarships kwa ajili ya wakufunzi wa vyuo vikuu vya binafsi ili wajiendeleze kielimu.
Ninachofahamu ni kwamba wanachuo wanapohitimu hapa wanaajiriwa mahali popote na hata
serikalini. Tunaomba tupewe nafasi ili wakufunzi wetu waweze nao kusoma zaidi kwa
kutumia scholarship za serikali.
Mhashamu Baba Askofu, changamoto
ni nyingi lakini kuna ambazo zingeweza kupungua makali kama serikali ingeona vyuo
hivi kama washirika wazuri na wenye nia njema ya kutayarisha wataalamu kwa ajili ya
Taifa letu na hivyo tupewe ushirikiano wa hali na mali. Ruzuku kwa maeneo kama ya
kutayarisha wataalamu wa sayansi ingekuwa uthubutu mkubwa wenye tija kwa upande wa
serikali na tunapenda kama Chuo kushauri hivyo.
Mwisho Mheshimiwa Mgeni
Rasmi, napenda kuwaasa wahitimu wetu waende kutimiza wajibu kama Watanzania wazalendo.
Mtu ameumbwa na ubinafsi wake lakini wasiuweke ubinafsi mbele bali watende kwa haki
wakimtegemea Mungu na kuendelea kusoma. Kusoma hakuna mwisho. Tafadhali wahitimu wetu
zingatieni maadili mema na kuendelea kuelimisha wengine bila kumwonea mtu aibu.
Kwa
wanachuo mnaobaki tafadhali muendelee kupenda kusoma kwa bidii. Naomba sana msaidiane,
mashauriane na kuelekezana ili wote muweze kumaliza masomo yenu vema. Mwenzenu akienda
njia isiyo sahihi msisite kumrekebisha kwa upendo na kumsaidia kuelewa wajibu wake
wa kusoma na kuishi katika maelekezo na maadili ya mtu mzima mwenye akili na utashi.
Mahangaiko na matatizo yatakuwepo lakini kwa njia ya taratibu ya kufuata taratibu
za Chuo zilizopo mtafaulu kuzitatua. Pendeni kuwa watu wa kufuata utaratibu na kutumia
busara katika kuamua na kuishi maisha yenu.
Mhashamu Baba Askofu, Mkuu wa Chuo,
naomba nikushukuru wewe binafsi kwa jitihada unazoweka katika kuchangia kukua kwa
elimu nchini. Wengine hapa hawatafahamu lakini naomba kwa ruhusa yako niwaeleze umma
huu kwamba wewe na marehemu Askofu Amedeus Msarikie ndiyo mlisimamia kuanzishwa kwa
vyuo vikuu vya Kikatoliki Tanzania (vikiwemo Mt. Augustino, Bugando, Ruaha ambacho
kiko Jimboni kwako na MWUCE). Aidha shukrani nyingi ziende kwa Mababa Askofu wa Baraza
la Maaskofu Katoliki kwa ushupavu na uthubutu wao wa kuwa na vyuo ili kusaidia Taifa
la Tanzania likue kimaendeleo. Mchango wa vyuo hivi ni mkubwa sana kwa Taifa Baba
Askofu.
Mwisho kabisa nikushukuru tena Baba ASKOFU KWA KUTOLEA MUDA WAKO KUJA
KUWATUNUKIA WAHITIMU WETU VYETI VYAO. AHSANTE SANA BABA ASKOFU. KARIBU SANA MWUCE
NA JISIKIE NYUMBANI. Fr. Philbert Vumilia Mkuu wa Chuo 02-11-2013