2013-11-05 13:51:24

Ban Ki moon na Jim Yong Kim watembelea Sahel


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon na Rais wa Benki ya Dunia Jim Yong Kim, Jumatatu walianza ziara ya pamoja kutembelea Mkoa wa Sahel Afrika Kaskazini.
Kufuatia ziara hii ya kihistoria ya viongozi hao wawili , Benk ya Dunia na Umoja wa Ulaya , Jumatatu uliahidi kutoa kiasi cha $bilioni 8.2 kwa ajili ya kukuza uchumi na kupambana na ufukara katika eneo la Sahel. EU ikiahidi msaada wa $6.7 biliioni katika kipindi cha miaka saba ijayo , na benk ya dunia itatoa msaada wa dola Billioni $1.5 katika kipindi cha miaka miwili.
Katika ziara hiìi , viongozi hawa kwa pamoja wanazuru Mali, Niger, Burkina Faso na Chad. Na mara walipowasili Bamako Katibu Mkuu Ban Ki mon, alizungumza na waandishi wa habari kuelezea kwa nini yeye na viongozi wengine wa dunia, wanakwenda katika ukanda wa Sahel, pamoja, ambako watahudhuria Mkutano wa Mkoa wa Mawaziri unaofanyika Bamako Mali.
Viongozi wengine wa ngazi ya juu wanaoshiriki katika ziara hii ni pamoja na Andris Piebalgs , Kamisheni katika Tume ya Umoja wa Ulaya kwa ajili ya Maendeleo , pia Nkosazana Dlamini Zuma , MwenyekIti wa Tume Tendaji ya Umoja wa Afrika, na Rais Donald Kaberuka , wa Benk ya Maendeleo ya Afrika.
Ban na Yong Kim wamewasili Mali wakionyesha kujali changamoto za kutisha zinazo jitokeza katika eneo hili, licha ya maafa ya kihali pia kuna mauaji ya makusudi kama ilivyofanyika kwa waandishi wawili wa Kifaransa waliouawa hivi karibuni. Wameonyesha kishawishi chao kwamba, mduara huu wa kipeo katika eneo la Sahel, unaweza kuvunjwa na mkoa huo kusonga mbele kutokana hali za wasiwasi na kuwa na uhakika wa maisha na maendeleo.
Mkoa wa Sahel ni eneo kame Kusini mwa jangawa la Sahara linalotambaa Kaskazini mwa Afrika tangu Mauritania hadi Eritrea, ambako, katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, limekuwa na ukame wa kukithiri kwa zaidi ya mara tatu, ikitishia maisha ya watu zaidi ya millioni 11 wa eneo hilo, hasa kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano wapatao milioni tano.









All the contents on this site are copyrighted ©.