2013-11-04 11:48:07

Sikiliza "The Original Comedy" ya Zakayo mtoza ushuru aliyeparamia Mkuyu ili kumwona Yesu!


Umoja wa Wanafunzi Wakatoliki Watanzania wanaosoma mjini Roma pamoja na watanzania katika ujumla wao, Jumapili iliyopita, tarehe 3 Novemba 2013 waliadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya kuwakaribisha wanafunzi wapya, kumkumbuka na kumwombea Mwl. Julius Kambarage Nyerere pamoja na kuungana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika Maandalizi ya Kufunga Mwaka wa Imani, huko Bagamoyo, Jumapili tarehe 10 Novemba 2013. RealAudioMP3

Ibada hii ya Misa Takatifu iliongozwa na Mheshimiwa Padre Alcuin Nyirenda. OSB na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa Mapadre, Watawa, Waseminari na Waamini walei. Katika mahubiri yake, Padre Nyirenda aligusia kwa namna ya pekee vituko vya maisha ya Zakayo; tajiri na mkuu wa watoza ushuru akikwea juu ya Mkuyu kwani alitamani kumwona Yesu.

Licha ya mali na utajiri; cheo na dhamana aliyokuwa nayo ndani ya Jamii, bado alikosa amani, utulivu wa ndani na furaha hadi pale alipokutana na Yesu, akamkirimia: amani, furaha na wokovu! Akamwonjesha huruma na upendo wa Mungu kwa kumwita kwa jina!









All the contents on this site are copyrighted ©.