2013-11-04 15:10:47

Marais wapya wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni


Wajumbe wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni, WCC, Jumatatu tarehe 4 Novemba 2013 wamefanya uchaguzi wa Marais kutoka sehemu mbali mbali za dunia wanaounda kanda za Uongozi. Mkutano huu umefanyika katika kikao cha faragha, katika mkutano mkuu wa kumi wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni unaoendelea mjini Busan, Korea ya Kusini.

Marais waliochaguliwa wanadhamana ya kuhamasisha majadiliano ya kiekumene miongoni mwa Makanisa pamoja na kutafsiri kwa vitendo maamuzi ya mkutano mkuu wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni kadiri ya maeneo wanayowakilisha. Mkutano huu pia unatarajiwa kuwachagua wajumbe wa Kamati kuu ya Baraza la Makanisa Ulimwenguni.

Marais waliochaguliwa ni pamoja na:
1. Afrika: Rev. Dr. Mary Anne Plaatjies Van Huffel, kutoka Afrika ya Kusini.
2. Asia: Prof. Dr. Sang Chang, kutoka Korea.
3. Ulaya: Askofu mkuu Anders Wejryd kutoka Sweden.
4. Amerika ya Kusini na Caribbean: Rev. Gloria N. U. Alvardo, kutoka Colombia.
5. Amerika ya Kaskazini: Askofu Mark Macdonald kutoka Canada.
6. Visiwa vya Pacific: Rev. Dr. Mele'ana Puloka kutoka Visiwa vya Tonga.
7. Waorthodox wa Mashariki: Patriaki John X kutoka Antiokia.
8. Waorthodox wa Magharibi: Patriaki Karekini II kutoka Armenia.







All the contents on this site are copyrighted ©.