Makardinali 7 na Maaskofu 136 wamefariki dunia katika kipindi cha Mwaka 2012-2013
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 4 Novemba anatarajiwa kuadhimisha Ibada
ya Misa Takatifu kwa ajili ya kuwakumbuka na kuwaombea Marehemu Makardinali na Maaskofu
waliofariki dunia katika kipindi cha Mwaka 2013. Ibada hii itafanyika kwenye Kanisa
kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican majira ya asubuhi. Katika kipindi hiki, Makardinali
7 na Maaskofu 136 wamefariki dunia, kati yao 17 ni kutoka Barani Afrika.
Kutoka
Afrika, Kanisa limempoteza Kardinali Medardo Joseph Mazombwe, Askofu mkuu mstaafu
wa Jimbo kuu la Lusaka, Zambia aliyefariki dunia hapo tarehe 29 Agosti 2013.
Kanisa
Barani Afrika linaomboleza vifo vya Maaskofu wafuatao: 1. Askofu mkuu mstaafu
Henry Ernest Karlen, Jimbo kuu la Bulawayo, Zimbabwe. 2. Askofu Aloysius Balina,
Jimbo Katoliki Shinyanga, Tanzania. 3. Askofu mstaafu Patrick Francis Sheehan wa
Jimbo Katoliki Kano, Nigeria. 4. Askofu mkuu Ambrose Madtha, Balozi wa Vatican
Pwani ya Pembe. 5. Askofu mstaafu Augugustin Sagna wa Jimbo Katoliki Ziguinchor,
Senegal. 6. Askofu mstaafu John Martin Darko wa Jimbo Katoliki Sekondi-Takoradi,
Ghana. 7. Askofu Joseph O. Egerega, wa Jimbo Katoliki Bomadi, Nigeria. 8. Askofu
mstaafu Ignace Sambar Talkena wa Jimbo Katoliki la Kara, Togo. 9. Askofu mstaafu
Amedeus Msarikie wa Jimbo Katoliki Moshi, Tanzania. 10. Askofu mstaafu Gerald Sithunywa
Ndlovu wa Jimbo Katoliki la Umzimkulu, Afrika ya Kusini. 11. Askofu mstaafu Akio
Johnson Mutek wa Jimbo Katoliki Torit, Sudan ya Kusini. 12. Askofu mstaafu Felix
Ramananarivo wa Jimbo Katoliki Antsirabè, Madagascar. 13. Askofu mkuu mstaafu Dominic
Kodwo Andoh, Jimbo Katoliki la Accra, Ghana. 14. Askofu mkuu mstaafu Michael Kpakala
Francis, Jimbo kuu la Monrovia, Liberia. 15. Askofu mstaafu Luis Gonzaga Ferreira
da Silva, Jimbo Katoliki Lichinga, Msumbiji. 16. Askofu mstaafu Bernardo Filipè
Governo wa Jimbo Katoliki Quelimane, Msumbiji. 17. Askofu mstaafu Raymond Mwanyika
wa Jimbo Katoliki Njombe, Tanzania.
Hii ndiyo orodha ya Makardinali na Maaskofu
waliofariki dunia hadi kufikia tarehe 2 Novemba 2013 wakati tukiwa tunaandika taarifa
hii.
Raha ya milele uwape Ee Bwana na Mwanga wa Milele uwaangazie, wapumzike
kwa Amani, Amina.