2013-10-31 15:22:57

Salaam za Papa Francisko kwa Mkutano Mkuu wa WCC : Aomba mshikamano wa dhati.



Papa Francisko ametoa wito kwa Wakristo wote , kuimarisha maombi, sala na ushirikiano, kwa ajili huduma ya Injili. Wito huo umo katika barua yake kwa washiriki wa Mkutano wa Kumi Mkuu wa Baraza la Makanisa Duniani, unaofanyika Busan, Korea ya Kusini.
Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kukuza Umoja wa Kikristo , Kardinali Kurt Koch, Jumatano alisoma barua hiyo ya Papa , ambamo anawahimiza Wakristo wote, kuona kwamba, wameitwa kuwafikia wale ambao wanajikuta wamewekwa pembezoni na jamii hasa iliyoendelea. Na kwamba, Wakristu kama familia ya Mungu , wanapaswa kuonyesha mshikamano na wale wanaoishi mazingira magumu zaidi wanawake kwa wanaume, watu maskini, walemavu, hata wale ambao bado kuzaliwa, wagonjwa, wahamiaji na wakimbizi , wazee na vijana ambao hawana ajira.

Papa Francisko ameitumia nafasi hii pia kutoa shukurani za dhati kwashiriki wa mkutano huu, wa Busan, na kwa namna ya pekee kwa Katibu Mkuu , Dr Olav Fykse Tveit , na wawakilishi ya jamii ya Kikristo. Papa amewahakikishia sala zake na ukaribu wake wakati huu wa mkutano na pia katika uwajibikaji wa kanisa Katoliki kwenye mwendelezo wa ushirikiano wa muda mrefu na na Baraza la Makanisa la Dunia.
Papa anasema, mandhari ya Mkutano huu wa Busan, ni "Mungu wa Maisha, tuongoze katika Haki na Amani" tayari ni ombi kwa Utatu Mtakatifu wa Mungu, ambaye huvileta viumbe vyote katika utimilifu, kwa njia ya nguvu ya ukombozi ya Msalaba wa Yesu Kristo na kwa namna nyingi za zawadi za Roho Mtakatifu. Kwa hakika , kila mahali ambapo zawadi ya Maisha huheshimiwa, haki na amani kutawala , mahali hapo upo Ufalme wa Mungu na uwezo wake uko tayari kufanya kazi.
Kwa sababu hii, Papa ameonyesha tumaini lake kwamba, uwepo wa mkutano huu wa Busan, utaweza kusaidia kuimrisha dhamiri ya wafuasi wa Kristu kattika maombi na ushirikiano katika huduma, na mwingiliano wa utendaji katika familia ya binadamu, kwa ajili ya ufanikisha mazuri kwa watu wote.
Katika dunia hii ya utandawazi Papa ameendelea,Wakristu wanatakiwa kushuhuduia kwa pamoja , heshima ya utu wa Mtu aliyopewa na Mwenyezi Mungu, na kukuza utamaduni na sheria za kijamii zinazomruhusu kila mwanadamu na kukuza ufanisi katika mazingira ya kitamaduni, kijamii na kisheria, ili kuwezesha watu binafsi na jamii kwa ujumla kukua katika uhuru, na ambao ni msaada msingi kwa familia, kujenga jamii katika mshikamano thabiti katika majiundo na utoaji wa elimu ni muhimu kwa vijana , na kwa ajili ya kuthamini utendaji usioweza kukwepa wa uhuru wa kidini. Na kwa uaminifu wa injili, na katika kukabiliana na mahitaji ya dharura ya wakati huu wetu, tunatakiwa kuwafikia wale ambao wameachwa pembezoni na jamii na kuonyesha mshikamano nao, hasa wale wanaoishi katika mazingira magumu, wake kwa waume, maskini, walemavu, na wale ambao hawajazaliwa, wagonjwa, wahamiaji na wakimbizi , wazee na vijana ambao hawana ajira.

Kwa ufahamu kwamba, wa moyo wa kiekumeni unabaki kuwa uongofu wa kweli takatifu ( taz. Unitatis Redintegratio , 8) , Papa anasali kwa ajili ya Mkutano Mkuu huo, ili uweze kuchangia katika kutoa msukumo mpya wa uhai na matazamio katika sehemu ya uwajibikaji wote wa mchakato mtakatifu unaotafuta Umoja kamili wa Wakristu , katika uaminifu wa mapenzi ya Bwana kwa Kanisa lake (taz. Yn 17:21 ) na katika uwazi wa unaokuzwa Roho Mtakatifu.
Kwao wote washiriki wa Mkutano huu wa Busan , Papa amewapa Baraka zake za Kitume na kuwaombea Baraka tele za Mwenyezi Mungu, chanzo cha maisha yote na kila zawadi ya kiroho.









All the contents on this site are copyrighted ©.