Rais Putin kukutana na Papa Francisko mwishoni mwa Mwezi Novemba?
Serikali ya Russia inaangalia uwezekano wa Rais Vladimir Putin kukutana na kuzungumza
na Baba Mtakatifu Francesko, mwishoni mwa Mwezi Novemba, wakati Rais wa Russia atakapokuwa
nchini Italia kwa mwaliko wa Serikali ya Italia. Kama mipango hii itakwenda kadiri
inavyosikika kwa sasa, hii itakuwa ni mara ya kwanza Rais wa Russia kukutana na kuzungumza
na Baba Mtakatifu.
Shirika la Habari la Zenith linabainisha kwamba, kwa sasa
Ikulu ya Russia inaendelea kufanya mazungumzo na Ikulu ya Italia kuhusu ratiba na
uwezekano wa viongozi hawa wawili kukutana. Italia na Russia itakuwa na mkutano wa
pamoja mjini Trieste mwishoni mwa Mwezi Novemba na baadaye ujumbe wa Russia utatembelea
pia mjini Roma.