Papa Francisko asema, Matumaini ni zawadi itokayo kwa Roho Mtakatifu
Mapema Jumanne Baba Mtakatifu Francisko , akiongoza Ibada ya Misa katika Kanisa dogo
la Mtakatifu Marta, Vatican, alihimiza Wakristu kuwa na tumaini thabiti kwa Kristu,
kwa kuwa tumaini ni zawadi kutoka kwa Roho Mtakatifu. Papa alielezea maana ya
kweli ya tumaini akisema kwamba, tumaini la Mkristu ni zaidi ya matumiani ya kawaida,
kwa kuwa, kutumaini katika Kristu ni kutarajia zawadi itokayo kwa Roho Mtakatifu
, ni fumbo jipya ambalo kamwe halimtelekezi mtu.
Baba Mtakatifu Francisko
alieleza kwa kurejea maneno ya Mtakatifu Paulo yanayosema, kumtumaini Kristu ni
kuwa na tumaini lisilofadhaisha, au kutelekeza, kwa sababu ni zawadi itokayo kwa
Roho Mtakatifu. Mtakatifu Paulo anaendelea kutuambia kwamba tumaini hili lina jina
nalo ni Kristo.
Papa aliendelea kufafanua maana ya matumaini, akisema hujenga
aina ya mvuto unaoelekea katika ufunuo wa Yesu Kristo , unao elekea katika furaha
ya kweli ambayo ni uzima wa milele .
Na akirejea fadhila ya imani, matumaini
na mapendo , Papa alisema kuwa mara nyingi fadhila ya matumaini ni unyenyekevu zaidi
katika mambo haya tatu , kwa sababu , tumaini limefichika katika siri ya maisha.
Mtakatifu Paulo anasema : ni motomoto wa fadhila katika matumaini ya Ufunuo, na wala
si jambo la kufikirika.
Papa aliendelea kufundisha kwamba, Yesu, Tumaini
la Mkristu, hubadilisha yote katika maisha. Hivyo matumaini yanakuwa ni muujiza wa
mara kwa mara. Muujiza katika kile anachokifanya Yeye katika Kanisa lake, muujiza
wa kufanya yote kuwa mapya. Na ni hivyo ndivyo, anavyo fanya katika maisha yangu,
katika maisha yako na katika maisha yetu wote. Yeye hujenga na kukarabati. Na hutenda
kwa haki kwa kuwa yeye ni tumaini la kweli. Kristo, ni Yeye anaye badilisha kila
kitu katika maajabu ya Uumbaji. Ni Yeye kwa sababu ndiye tumaini letu, lisilo jishaua
kwa sababu Yeye ni mwaminifu, na hawezi kujikana mwenyewe. Na hivyo Yeye ni fadhila
na tumaini letu la kweli.
Na alihitimisha kwa kuwakumbusha Wakristo wote,
kumgeukia Mama Bikira Maria , ambaye alibaki na tumaini hata wakati wa giza la kifo
cha mwanae Msalabani hadi kufufuka kwake . Ni tumaini lililojaa ndani ya moyo wake
lililomfariji wakati wa giza hicho katika maisha yake.lakini matumaini yalifanya upya
kila kitu. Papa alieleza na kutolea ombi kwa Mwenyezi Mungu, ili tupate neema
hii ya moyo wa matumaini siku zote.