Papa afafanua kiini cha Maadhimisho ya Siku ya Watakatifu wote na siku ya Marehemu
wote.
BabaMatakatifu Francisko akiendelea kutoa tafakari juu ya sala ya Nasadiki, kwa Jumatano
hii, alilenga zaidi katika usharika na Watakatifu, kama Kateksimu ya Kanisa Katoliki
inavyotukumbusha sisi kwamba, usharika huu ni kwa Mambo Matakatifu na kati ya watu
Watakatifu (No. 948 ).
Papa alizama zaidi katika sehemu ya Pili ya kuw ana
usharika na Marehemu Watakatifu , ukweli unaohitaji ufafanuzi zaidi katika imani
yetu, akieleza pia kwamba, hutukumbusha pia kwamba, hatuko pweke, lakini kuna uwepo
wa usharika wa maisha kwa wale wanaokuwa wa Kristu. Usharika mmoja unaoundwa na imani
, katika ukweli wake, neno hili Watakatifu hurejea wale wanao mwamini Yesu Kristu
kuwa ndiye Bwana wa Maisha na hivyo humwilishwa kwake Yeye ndani ya kanisa kupitia
ubatizo. Na kwa namna hiyo , Wakristu wa kwanza waliitwa pia Watakatifu.
Papa
aliendelea kufundisha , Usharika wa Watakatifu ni kina halisi cha maana ya Kanisa
kwa sababu kama wakristu kupitia Ubatizo , tunafanywa kuwa washiriki wa maisha ya
usharika mmoja na upendo wa Utatu Mtakatifu. Na hivyo sote tunaunganishwa mmoja kwa
mwingine na kiungo cha ubatizo katika Mwili wa Kanisa. Na kupitia usharika huu wa
kidugu, tunawekwa karibu zaidi na Mungu, na tukitakiwa kusaiidiana mmoja kwa mwingine
kiroho.
Papa alieleza na kuirejea Injili Yohana ambayo inasema kwamba , kabla
ya mateso yake, Yesu aliomba kwa Baba kwa ajili ya umoja kwa wanafunzi wake kwa maneno
haya : “Naomba ili wote wawe kitu kimoja kama wewe, Baba , ulivyo ndani yangu , nami
ndani yako. Naomba wawe kitu kimoja kusudi ulimwengu upate kuamini kwamba wewe ndiye
uliyenituma "( 17:21). Kanisa , katika kweli yake kamili , ni usharika na Mungu ,
usharika wa upendo na Kristo na Baba katika Roho Mtakatifu shina la usharika huo.
. Uhusiano huu baina ya Yesu na Baba ni dhamana kati ya Wakristo, iwapo pia sisi tumo
ndani yake katika umoja huu, na tanuru la moto huu wa upendo katika Utatu Mtakatifu,
basi tunaweza kweli kuwa na moyo na roho moja kati yetu kwa sababu upendo wa Mungu
unauguza ubinafsi wetu , chuki zetu, utengano na miganyiko yetu ya ndani na nje.
Papa
Francisko amesema, iwapo ushariki huu chanzo chake ni mzizi wa upendo ambao ni Mungu,
basi pia kuna sababu za kufanya hima kutoa jibu landiyo katika muungano huu na Mungu,
maisha ya ushirika wa udugu unaoongoza katika kuwa msharika na Mungu.
Hii
ni sehemu ya pili ya usharika, ambayo Papa alitoa msisitizo zaidi, kuwataka watu
wa Mungu,kupta uelewa mpana kwamba, imani yetu inahitaji msaada wa wengine , hasa
katika nyakati ngumu. Alisema, tazama pia jinsi ilinavyokuwa vizuri kutoa msaada
kwa mwingine katika maajabu haya ya imani! Papa alieleza kukemea mwelekea kukubatia
tabia ya kutaka kujifungia binafsi, hata katika mazingira ya kidini, kiasi kwamba,
inakuwa hata vigumu kwa wengine, hata kuomba msaada wa kiroho, kwa wale wenye uzoefu
katika maisha haya ya Kikristu.
Papa alihimiza katika nyakati hizi ngumu
ni muhimu kuwa imani kwa Mungu kupitia sala, na wakati huo huo, ni muhimu kupata
ujasiri na unyenyekevu kuwa wazi kwa wengine. Papa amekumbusha ushirika wa watakatifu
ni familia kubwa, ambapo vipengele vyote ni kusaidia na kusaidiwa yaani kusaidiana
mmoja kwa mwingine. Kushirkiana na wengine katika parokia zetu, katika vyama , jumuiya,
harakati na vikundi, kama sehemu ya maisha katika safari yetu ya imani, ni kutochoka
kuomba msaada wa maombezi na faraja ya kiroho. Ni wakati wetu wa kusikiliza na kuwasaidia
wale ambao hawaja jiunga nasi katika safari hii.
Papa alikamilisha Katekesi
yake kwa kuchambua kipengele kingine cha usharika wa watakatifu, akisema kwamba,
ushariki wa wakatifu huenda zaidi ya maisha ya dunia, inakwenda zaidi ya kifo kwa
kuwa huduma milele. Usharika wa kiroho tunaopokea wakati wa Ubatizo hauvunjwi na kifo
, lakini umeinuliwa na ufufuko wake Kristu, unao ipeleka roho katika mapito ya utimilifu
wa maisha ya milele.
Papa aliendelea kubaini kwmba, kuna dhamana ya kina na
isiyokuwa na mwisho kati ya wale ambao bado mahujaji katika dunia hii na wale ambao
wamevuka kizingiti cha kifo na kuingia katika umilele. Wote hao huuundwa wakati wa
ubatizo hapa duniani,na nafsi hutakatifushwa toharani na kufanywa wenye heri, kuingia
katika makazi ya mbinguni ambako ni makazi ya familia moja kubwa. Ushirika huu kati
ya nchi na mbinguni ni barabara ya maombezi , ambayo ni aina ya juu ya mshikamano,
na pia ni msingi wa maadhimisho ya kiliturujia ya Watakatifu wote na Maadhimisho ya
Marehemu wote kama itakavyokuwa siku chache zijazo.
Papa alimalizia kwa kumtaka
kila mmoja alifurahie fumbo hili , na kumwomba Bwana neema zake , ili tuweze kuwa
karibu zaidi naye na katika usharika na waamini wote, wake kwa waume ndani ya kanisa. Wito
wa Kuombea Iraki Baada ya Katekesi, Papa akisalimia makundi mbalimbali,
pia alilitaja kundi la mahujaji kutoa Iraki ambao walikuwa wakiwakilisha makundi mbalimbali
ya kidini, toka yanayojionyesha kama ni utajiri wa Ukristu katika taifa la Iraki .
Kundi hili liliongozwa na Kardinali Tauran Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya majadiliano
na dini zingine. Papa alitoa wito kwa watu wote kukumbuka kuliombea taifa la Iraki
ambalo kila kukicha hukumbana na majanga ya fujo na ghasi za kusitisha zinazofaywa
na makundi mabalimbali. Tusali ili Iraki ipate kurejea katika njia ya majadiliano,
maridhianao , amani, umoja na utulivu wa kudumu kitaifa.