2013-10-29 15:43:51

Vatican yapanda hadhi katika kipimo cha uwazi kwenye masuala ya fedha


Wakala wa Kujitegemea katika upimaji wa viwango vya uadilifu kwenye masuala yanayohusiana na fedha na Benki “The Standard Ethics Rating (SER)”, Jumatatu walitangaza kupandisha hadhi Nchi ya Jiji la Vatican katika kipimo cha ubora wa usimamizi na uwazi kwenye masuala ya fedha .

Shirika hili la SER, ni chombo kinacho pima hali katika masuala ya uendelevu , wajibu wa kijamii , utawala bora na mazingira yanayohusiana na masuala ya fedha haswa uhamishaji wa fedha kutoka akaunti moja hadi nyingine.
Taarifa inasema, Vatican imeonyesha jitihada chanya na endelevu, katika kipimo cha uboreshaji wa maadili katika mifumo yake ya fedha na jamii, kama matokeo ya kazi na takwimu za kisayansi zilizo fanywa hapa na pale katika dunia ya uchumi kwenye uhusiano wa kanuni za maadili zinazozingatiwa na mashirika makubwa ya kimataifa.

Na kwamba, SER, tangu ilipopewa mtazamo chanya Julai iliyopita , kwa kazi zake za kusimamia masuala ya fedha Vatican, Jiji la Vatican limefanikisha matwaka ya kimataifa yanayo dai uwazi zaidi katika akaunti za Vatican na taasisi zake za kifedha.

Na pia inafafanua kwamba , Vatican ilitakiwa kuchukua hatua muhimu dhidi ya utakatifushaji fedha wa haramu, au fedha kutumika katika matendo haramu au ufadhili wa ugaidi kwa fedha zinazotoka au kuingia katika Benk yaVatican au taasisi zake za fedha. Vatican imweze kuzingatia taratibu na vigezo vilivyo wekwa na Jopo la Utendaji la Kujitegemea”Financial Action Task Force” (Groupe d' Financière FATF - GAFI ) kama ilivyo pitishwa katika mapendekezo kutoka Idara Moneyval ya Baraza la Ulaya .

Aidha, ripoti inaeleza kwamba hatua muhimu zillizo chukuliwa, zimefanikishwa na Tume ya Kipapa kwa ajili ya utawala wa nchi ya Jiji la Vatican, kwa sheria yake namba XVIII ya Oktoba 8, 2013 . Sheria hii inafanikisha uwepo wa chombo kinachosimamia uwazi, usimamizi na utoaji wa taarifa za fedha . Sheria mpya ni matunda ya Katiba ya miaka michache iliyopita ya Mamlaka ya Habari wa Fedha ( AIF ).

Na pia kwamba, Mambo zaidi ya uwazi na ripoti na matamko , yamefanikisha uchapishaji wa Ripoti ya Mwaka ya Shughuli ya Fedha, na Mwaka wa kwanza wa AIF 2012, pia uchapishaji wa ripoti ya kila mwaka kwenye tovuti ya Benki ya Vatican ( Istituto kwa le Opere Religiose IOR ) iliyotoka tarehe 1 Oktoba 2013.








All the contents on this site are copyrighted ©.