2013-10-28 15:56:33

Papa -Yesu anaendelea kuomba kwa ajili yetu


Yesu anaendelea kuomba kwa ajili yetu, akimwonyesha Baba thamani ya wokovu wetu, tulioupta kupitia vidonda vyake vya Msalabani. Maneno haya ni msisitizo wa mahubiri ya Papa Francisko, alioutoa katika Ibada ya Misa, mapema Jumatatu hii. Ibada aliyoiongoza katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta mjini Vatican. Homilia hiyo iliangalishwa katika Injili ya siku kwa ajili ya maadhimisho ya Watakatifu Simon na Yuda Mitume .

Kiini cha homilia ya Papa , kililenga zaidi katika kifungu za Injili ambamo Yesu aliutumia muda wote wa usiku katika maombi , kabla ya kuchagua mitume wake kumi na wawili.Yesu anatengenza timu yake, Papa alisisitiza. Na mara baada ya tukio hili, akiwa amezungukwa na umati mkubwa wa watu, waliofika kumsikiliza na kuponywa Naye, kwake Yeye ambaye mlitoka nguvu za uponyaji kwa wote.
Papa ametafakari Injili hiyo akisema, hapa tunaona mambo matatu. Yesu katika mahusiano na Baba yake, Yesu na Mitume wake na Yesu na watu. Yesu aliomba kwa Baba kwa ajili ya Mitume na kwa ajili watu. Na hata leo hii , bado anaomba kwa ajili ya wale wanaomwomba Mungu na yuko pamoja na wale wanaomwomba Mungu.
Papa aliwahimiza waliokuwa wakimsikiliza kuwa na imani kwamba,Yesu tunayesali mbele yake ndiye aliyetukomboa kwa sadaka ya maisha yake, na kutuhalalisha sisi kuitwa wana wa Mungu, kwa mastahili yote. Na kwa sasa ameondoka lakini bado anaomba kwa ajili yetu. Papa alihoji iwapo Yesu ni i roho? Na kutoa jibu kwamba, la, Yesu si Roho, bali Yesu ni mtu , mtu aliyemwilishwa na kuwa na mwili kama wetu lakini katika utukufu wake Mungu. . Yesu ana majeraha kwenye mikono , miguu, ubavu , na wakati anaomba kwa Baba, anaonyesha thamani ya haki ya kuomba kwa ajili yetu, kama akisema, " Baba, wote ulionipatia asipotee hata mmoja wao" hivyo tunaimani kwamba waamini hakuna atakayepotea"

Yesu pia ni kichwa cha maombi yetu, kwa sababu ni yeye aliomba kwanza, kama ndugu yetu na binadamu kama sisi, na bado anatuombea.

Papa alitoa wito kwa wote , kumwombea pia akisema, ee Bwana, Wewe ni mwombezi wangu. Alirudia kusisitiza, Yesu anaomba kwa ajili yangu, anaomba kwa sisi wote na anaomba kwa Baba ushujaa, akionyesha vidonda vyake kuwa dhamana ya haki yetu kuitwa wana wa Mungu. Papa amemtaka kila muumini afikiri sana kuhusu hili, na kumshukuru Bwana kwa wema wake uliotupa stahili hii. Asante kwa ndugu yetu anayejumuika nasi katika kuomba kwa ajili yetu. Maombezi kwa ajili yetu.
Papa anasemqa, basi yatupasa sisi pia kuzungumza na Yesu, na kumwambia: Bwana, Wewe ni mwombezi wangu , na mwokozi wangu, uliyenipa mastahili ya haki. Katika maombi yetu , tukabidhi kwake yeye Mwombezi wetu, matatizo yetu, maisha yetu, mambo mengi yote kwake, ili ayafikishe kwa Baba , aliyemtuma yey kuja duniani kutukomboa dhdi ya mwovu .







All the contents on this site are copyrighted ©.