2013-10-26 13:59:20

Viongozi wapongeza uhusiano mzuri kati ya Kanisa na Serikali nchini Panama


Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi, tarehe 26 Oktoba 2013 amekutana na kuzungumza na Rais Riccardo Alberto Martinelli Berrocal wa Panama na baadaye wamekutana pia na Askofu mkuu Dominique Mamberti, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.

Viongozi hawa wamezungumzia hali ya maisha nchini Panama na Jumuiya ya Kimataifa kwa ujumla kuhusu masuala ya kijamii na mipango ya maendeleo endelevu. Viongozi hawa wawili wamepongeza uhusiano mzuri uliopo kati ya Kanisa na Serikali kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wananchi wa Panama.

Rais wa Panama amemzawadia Baba Mtakatifu Francisko Sanamu ya Bikira Maria wa Antiqua ambayo imepamba tayari kwenye bustani za mji wa Vatican. Baadaye viongozi hao, wamegusia pia masuala mbali mbali ya kimataifa.







All the contents on this site are copyrighted ©.