Askofu msaidizi Anastacio Kahango ang'atuka kutoka madarakani; Monsinyo Aldo Giordano
ateuliwa kuwa Balozi mpya Bolvia na Venezuela
Baba Mtakatifu Francisko tarehe 26 Oktoba 2013 amekubali ombi la kung'atuka kutoka
madarakani lililowasilishwa kwake na Askofu msaidizi Anastacio Kahango wa Jimbo kuu
la Luanda, Angola mintarafu sheria za Kanisa namba 411 na 401ยง 1 za Sheria za Kanisa.
Wakati huo huo, Baba Mtakatifu Francisko amemteuwa Monsinyo Aldo Giordano
kuwa Balozi mpya wa Vatican nchini Bolvia na Venezuela na kumpandisha hadhi kuwa ni
Askofu mkuu. Kabla ya uteuzi huu, Askofu mkuu Mteule Giordano alikuwa ni m wakilishi
maalum wa Vatican kwenye Umoja wa Ulaya. Alizaliwa tarehe 20 Agosti 1954 mjini Cuneo,
Italia.
Baada ya majiundo na malezi yake ya Kikasisi, akapadrishwa hapo tarehe
28 Julai 1979. Askofu mkuu mteule anauzoefu mkubwa katika taaluma kama Jaalimu la
Falsafa. Amekwisha wahi kuteuliwa kuwa Katibu mkuu wa Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu
Katoliki Ulaya kwa takribani miaka 13.