2013-10-25 12:14:26

Wakristo wataendelea kutangaza Injili licha ya mauaji, nyanyaso na dhuluma za kidini!


Mauaji ya viongozi wa Kanisa, dhuluma na nyanyaso dhidi ya Wakristo Afrika Mashariki ni vitendo ambavyo kamwe havitaweza kuzimisha moto na ari ya utangazaji wa Habari Njema Afrika Mashariki na badala yake, damu ya Wakristo hao ni mbegu ya kueneza imani sehemu mbali mbali za dunia.

Ni ushuhuda uliotolewa hivi karibuni na viongozi wa Madhehebu ya Kikristo mjini Mombasa kufuatia tukio la mauaji ya kinyama kwa wachungaji wawili mjini Mombasa, hivi karibuni. Viongozi wa kidini wanaitaka Serikali ya Kenya kuhakikisha kwamba, inalinda na kudumisha uhuru wa kuabudu sanjari na utawala wa sheria.

Viongozi hao wanasema, mauaji, mateso na dhuluma dhidi ya Wakristo hayatawafanya kuogopa kutangaza Habari Njema ya Wokovu na badala yake, wataendelea kuchochea moto wa Injili ili watu waweze kujenga utamaduni wa kuheshiana, upendo, haki, amani, msamaha, upatanisho na mshikamano wa kitaifa hata katika tofauti za kidini.







All the contents on this site are copyrighted ©.