2013-10-24 12:50:47

Dunia yaadhiimisha Siku ya Umoja wa Mataifa


Kila mwaka tarehe 24 Oktoba, ni Siku ya Umoja wa Mataifa. Ujumbe wa Katibu Mkuu wa umoja huo, Bwana Ban Ki Moon, kwa ajili ya maadhimisho haya amesema, siku hii inalenga kutoa utambuzi zaidi, jinsi gani chombo hiki cha thamani sana, hutoa mchango mkubwa katika udumishaji amani na maendeleo ya wakazi wote wa dunia. Na kwamba , siku hiii iliwekwa kama fursa ya kutafakari zaidi mipango kwa ajili ya mafanikio na maisha bora kwa siku za usoni.
Aidha katika ujumbe huo, ameitazama hali ya vita na mapigano yanayoendelea Syria akisema ni changamoto kubwa katika usalama na utulivu wa dunia, kwa wakati huu, mamillioni ya watu, kuishi kwa kutegemea msaada wa ubinadamu, kuokoa maisha yao.
Ban Ki moon ameonyesha kutambua juhudi za Watalaam wa umoja wa Mataifa wanao fanyakazi bega kwa bega na Shirika liloshinda Tuzo ya Heshima katika juhudi za kuzuia silaha za kemikali, ambao wanafanyakazi ya kuangamiza shehena ya kemikali hizo za hatari zilizo hifadhiwa Syria. Na kwamba, Umoja wa Mataifa unafanya pia jitihada kupitia msukumo wa kidiplomasia kufikisha mwisho wa kipindi kirefu cha mateso kwa watu wa Syria.
Ujumbe wa Katibu Mkuu, pia umezitaja changamoto zinazo pambana na ufanikishaji malengo ya Maendeleo na ustawi wa jamii, ukionyesha kutambua kwamba, umaskini umeweza kupunguzwa kwa nusu. Na kwa sasa kazi kubwa ni kudumisha msukumo na mshikamano huo katika ufanikishaji wa malengo ya Mandeleo yanayokamilika mwaka 2015, na pia kufikia makubaliano thabiti katika agenda ya kukabiliana na Mabadiliko ya tabia nchi .
Aidha amesema, kwa mara ingine tena mwaka huu, kumeshuhudiwa Umoja wa Mataifa ukijumuika pamoja kuzungumzia juu ya mizozo ya kutumia silaha, haki za binadamu , mazingira na masuala mengine . Na Umoja unaendelea kuonyesha kinacho takiwa zaidi ni ushirikiano , na unawezo wa kutenda zaidi, katika dunia ya leo, iliyounganishwa zaidi na yenye kuwa na lazima ya kushikamana zaidi.
Katibu Mkuu Ban Ki Moon amemalizia ujumbe wake na wito kwamba, katika Siku hii ya Umoja wa Mataifa , na tutoe ahadi ya kuyaishi mawazo yetu na kufanya kazi kwa pamoja, kwa ajili ya kufanikisha amani, Maendeleo na haki za binadamu.








All the contents on this site are copyrighted ©.