2013-10-19 15:06:24

Papa akutana na Tume ya Kimataifa kwa ajili ya kitabu cha Liturujia katika lugha ya Kiingereza.


(Vatican Radio) Papa Francisko Ijumaa ya 18 .10.13, alikutana na wajumbe wa Tume ya Kimataifa wanaoshughulika na kutafasiri Liturujia katika lugha ya Kiingereza(ICEL). Aliwaambia kwamba, matunda ya kazi yao imesaidia kuunda sala za maombi kwa Wakatoliki wengi.Wajumbe wa ICEL, walikutana Rome kwa lengo la kusherehekea maadhimisho ya miaka hamisini tangu kuanzishwa kwa tume hiyo.
Papa katika hotuba yake kwa wahudumu na wajumbe wa ICEL, ilianza kwa kutoa shukurani kwa Askofu Mkuu Arthur Roche , Katibu wa Shirika kwa ajili ya Ibada Takatifu na Nidhamu za Sakramenti , na Rais wa zamani wa ICEL . Na kupitia kwao Papa alipeleka salaam zake za matashi mema na shukurani kwa kwa Mabaraza ya Maaskofu waliyoyawakilisha na kwa washauri na wafanyakazi ambao hushirikiana nao katika kufanikisha kazi za Tume.

Tume hii ilianzishwa kama sehemu ya utekelezaji wa upya na mabadiliko makubwa katika mfumo wa liturujia kama ilivyotajwa katika Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, juu ya Liturujia Mungu. Kuundwa kwa ICEL pia ikawa ni moja ya ishara ya roho ya umoja wa Maaskofu, katika upatikanaji wa Katiba mpya ya Baraza, juu ya Kanuni Sadikifu za Kanisa (taz. . Lumen Gentium , 22-25 ).
Papa aliendelea kueleza kuwa maadhimisho ya miaka hamsini tangu kuundwa kwa tume hiyo , ni ishara ya kumshukuru Mungu kwa kazi zilizofanikishwa na Tume katika kipindi hiki cha miaka hamsini katika kutoa taratibu za Liturujia katika lugha ya Kiingereza, lakini pia katika kuendeleza utafiti , uelewa na matumizi ya utajiri wa Kanisa kisakramenti na milaza mapokeo.
Lydia O’Kane akiripoti juu ya ICEL, anasema, Kazi ya Tume pia zimetoa mchango mkubwa katika dhamira , utendaji na ucha Mungu , kama ilivyotakiwa na Baraza la Mtaguso Mkuu wa Pili , na kama Papa Benedict XVI alivyowakumbusha mara kwa mara, umuhimu wa kueleweka kwa undani zaidi katika misingi ya kuelewa siri ya fumbo la Ekaristi linaloadhishwa na mahusiano yake na maisha ya kila siku "( Sacramentum Caritatis , 52) . Papa Francisko aliwambia wajumbe wa ICEL kwamba, matunda ya kazi yako si tu yamesaidia wakatoliki kuweza kuunda maombi ya Wakatoliki mazuri zaidi , lakini pia Imechangia uelewa wa imani , kazi za kawaida za Padre, na moyo mpya katika utendaji wa utume wa Kanisa kwa kila muumini, kulingana na mafundisho ya Mtaguso. Kama Mwenye Heri Yohane Paulo II alivyosema, "watu wengi wameupokea ujumbe wa Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican,hasa kupitia mageuzi ya kiliturujia " ( Vicesimus Quintus Annus , 12).

Papa Francisko aliendelea kuishukuru Tume ya ICEL, kwa kuwezesha idadi kubwa ya waamini wa Kanisa Katoliki Duniani kote kuomba katika lugha yao mahalia, na pia katika kukuza umoja wa Kanisa katika imani na ushirika katika sakramenti, ambayo ina asili yake ni katika Utatu Mtakatifu Uliobarikiwa, ambao daima hupatanisha na kuongeza maana ya utajiri wa utofauti. Papa Francisko alionyesha tumaini lake kwamba, juhudi zao katika kutafasiri zitaendelea kuwa msaada wa kuelta ufahamu zaidi kama alivyohimiza Papa Paulo VI katika kueneza imani kupitia Misale , kwamba, licha ya utofauti mkubwa wa lugha, sala inabaki kuwa ni hiyohiyo moja, inayotolewa kama sadaka ya kukubalika kwa Baba yetu wa mbinguni , kwa njia ya juu Kuhani wetu Mkuu Yesu Kristo na katika Roho Mtakatifu. Papa Franisko alimalizia na kuwapa baraka zake za kitume kwa kazi yao muhimu.









All the contents on this site are copyrighted ©.