2013-10-18 13:58:13

Papa kuwaweka wakfu Maaskofu wakuu wawili, hapo tarehe 24 Oktoba 2013


Baba Mtakatifu Francisko kwa mara ya kwanza anatarajiwa kuwaweka wakfu Maaskofu wakuu wateule: Monsinyo Jean Marie Speich kutoka Jimbo Katoliki la Strasburg, Ufaransa na Monsinyo Giampiero Gloder kutoka Jimbo Katoliki Padova, Italia, hapo tarehe 24 Oktoba 2013, kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, majira ya jioni.

Itakumbukwa kwamba, Askofu mkuu mteule Jean Marie Speich alizaliwa kunako tarehe 15 Juni 1955. Baada ya masomo na majiundo yake ya kikasisi, akapadrishwa kunako tarehe 9 Oktoba 1982. Baba Mtakatifu Francisko akamteuwa kuwa Balozi wa Vatican nchini Ghana na hapo hapo kumpandisha cheo na kuwa Askofu mkuu tarehe 17 Agosti 2013.

Askofu mkuu mteule Giampiero Gloder alizaliwa kunako tarehe 15 Mei 1958. Baada ya masomo na majiundo yake ya kikasisi, akapadrishwa tarehe 4 Juni 1983. Baba Mtakatifu Francisko alimteua kuwa Balozi na Rais wa Baraza la Kipapa la Taasisi za Kikanisa, hapo tarehe 21 Septemba 2013.







All the contents on this site are copyrighted ©.