2013-10-16 08:28:49

Umuhimu wa sheria za kimataifa katika kuratibu mahusiano mbali mbali Barani Afrika!


Dr. Adelardus Kilangi mwenyekiti wa Tume ya Sheria za Kimataifa kwenye Umoja wa Afrika katika mahojiano maalum na Radio Vatican abainisha kwamba, Umoja wa Afrika katika miaka ya hivi karibuni umetambua umuhimu wa kuanzisha tume ya sheria za kimataifa. RealAudioMP3

Sheria za kimataifa ni muhimu sana katika kuratibu uhusiano kati ya nchi za Kiafrika na nje ya Bara la Afrika; mwendelezo wa utengamano kikanda; utekelezaji wa matamaniko makubwa ya Bara la Afrika na maendeleo endelevu kwa watu wake; ukuzaji na udumishaji wa demokrasia ya kweli. Haya yote anasema Dr. Kilangi ni mambo ambayo yanapaswa kuratibiwa na sheria za kimataifa.

Tume ya sheria za kimataifa ya Umoja wa Afrika inaundwa na Makamisheni kumi na mmoja kutoka katika nchi 54 zinazounda Umoja wa Afrika. Hii ndiyo tume inayojikita zaidi na zaidi katika utoaji wa ushauri wa sheria za kimataifa kwa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika. Hii ni fahari kwa Tanzania na kwa Chuo Kikuu cha SAUT cha Tanzania kupata mwakilishi katika tume hii ya kimataifa.







All the contents on this site are copyrighted ©.