2013-10-15 10:02:38

Wakala dhidi ya uhalifu waanzishwa na Uingereza


Kutokana na ongezeko la vitisho na vitendo vya kigaidi sehemu mbali mbali za dunia, Malkia wa Uingereza hivi karibuni alianzisha Wakala wa Kitaifa kwa ajili ya kupambana na Uhalifu, unaojulikana kama NCA, National Crime Agency. Wakala huu umepewa dhamana na jukumu la kudhibiti vitendo vya uhalifu nchini Uingereza pamoja na kuendelea kushirikiana na nchi 150 duniani. Wakala huu utakuwa pia na jukumu la kuangalia mwenendo wa Jeshi la Polis inchini Uingereza.

Wizara ya Mambo ya ndani ya Uingereza imebainisha kwamba, wakala huu utaungana pia na taasisi nyingine zilizopo nchini Uingereza katika kupambana na uhalifu wa kitaifa na kimataifa. Uhalifu kwa njia ya mitandao ya kijamii ni kati ya mambo yanayopewa kipaumbele kwa sasa sanjari na kulinda mipaka ya nchi pamoja na watoto. Kikosi cha Scotland Yard, maarufu katika masuala ya upelelezi nchini Uingereza kitaendelea kujikita katika mapambano dhidi ya ugaidi wa kitaifa na kimataifa.








All the contents on this site are copyrighted ©.