2013-10-15 10:17:54

Nchi za Kiafrika zatunisha misuri dhidi ya ICC!


Wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika katika mkutano wake uliofanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia mwishoni mwa juma, wameendelea kupinga mwenendo wa Mahakama ya uhalifu wa kimataifa dhidi ya ubinadamu iliyoundwa na Umoja wa Mataifa ili kuwashughulikia watu wanaojihusisha na mauaji ya kimbari, vita na uvunjaji wa haki msingi za binadamu.

Katika kikao cha mawaziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa, kama sehemu ya maandalizi ya mkutano wa wakuu wa nchi za umoja wa Afrika, viongozi hao waliutaka Umoja wa Mataifa kuangalia upya mwenendo wa mashitaka dhidi ya Omar Hassan Al Bashir wa Sudan, Rais Uhuru Kenyatta na William Ruto wa Kenya.

Viongozi wanaotuhumiwa hawapaswi kushitakiwa wakiwa bado madarakani na kwamba, Mahakama ya makosa ya kivita imeonesha mwelekeo potofu dhidi ya Bara la Afrika, tangu ilipoanzishwa kunako mwaka 2002 hadi wakati huu. Mahakama hii ilikuwa pamoja na mambo mengine kuhakikisha kwamba, inalinda na kutetea haki msingi za binadamu pamoja na kuendeleza mchakato wa upatanisho, lakini kwa bahati mbaya imegeuka kuwa ni chombo cha kisiasa dhidi ya Bara la Afrika na viongozi wake.

Hii ndiyo hali ya jumla inayosikika kutoka Barani Afrika. Viongozi kutoka Barani Afrika wanataka wapewe kinga dhidi ya njama za Mahakama ya uhalifu wa kivita wanapokuwa madarakani.








All the contents on this site are copyrighted ©.