Jihadharini na matapeli wakati wa Ibada ya kuwatangaza watakatifu Yohane Paulo II
na Yohane wa XXIII
Mama Kanisa anatarajiwa kuwatangaza Wenyeheri Yohane wa XXIII na Yohane Paulo II kuwa
watakatifu Jumapili ya tarehe 27 Aprili 2014, kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu
Petro mjini Vatican. Tukio hili linatarajiwa kuhudhuriwa na bahari ya watu kutoka
sehemu mbali mbali za dunia.
Vatican inapenda kuwatangazia waamini na watu
wote wenye mapenzi mema kwamba, katika Ibada ya Misa ya Siku hiyo, hakutakuwepo na
tiketi maalum kwa ajili ya kuhudhuria Ibada hiyo. Kila mtu atakuwa huru kuingia katika
Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro na viunga vyake kadiri ya nafasi itakavyoruhusu.
Vatican
pia inawataadharisha watu wasijekujikuta wanatapeliwa na makampuni ya kitalii kwa
kuwatoza fedha kwa ajili ya kushiriki katika Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya kuwatangaza
Wenyeheri Yohane wa XXIII na Yohane Paulo II kuwa watakatifu.
Mchezo kama
huu umewahi kufanyika katika matukio kama haya. Vatican inapenda pia kuwajulisha waamini
na watu wenye mapenzi mema kwamba, tiketi zinazotolewa kwa ajili ya kushiriki kwenye
Katekesi na Ibada zinazoendeshwa na Baba Mtakatifu ni bure na wala haziuzwi.