2013-10-15 15:35:54

Jifunueni katika umoja na mshikamano wa binadamu wote-Kardinali Tarcisio Bertone.


Jumapili Oktoba 13 2013, wakati Papa Francisko akiongoza Ibada ya Misa katika Kuu la Mtakatifu Petro na kuikabidhi dunia chini ya Moyo Mtakatifu sana wa Bikira Maria, nae Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu wa Nchi ya Vatican, na Jimbo Takatifu kwa ujumla, aliongoza Ibada ya Ekaristi katika Madhabahu ya Mama Yetu wa Fatima.

Taarifa inaeleza Jumamosi 12 Oktoba, Kardinali Tarcisio aliongoza maadhimisho ya kumbukumbu ya kupita miaka sitini ya Kanisa Kuu la Mama Yetu wa Rozari,alilo litaja kuwa ni Nyumba ya Mama, ambamo mahujaji hukusanyika kwa lengo la kukutana na Mwanae Yesu Kristu, anayewaalika katika njia ya uongofu, maisha ya kutembea katika njia isiyo ya udanganyifu , ila njia inayongoza katika utulivu kamili wa maisha si ya kiroho tu lakini hata kimwili. Ni kama ilivyokuwa kwa Zakayo aliyeketi kwa utulivu juu ya matawi ya mkuyu ili apate kumwona Kristo akipita na kuwa kinyume chake, Bwana anapofikia, alimwita zakayo na kumtaka ateremke haraka maana alipenda kula chakula katika nyumba yake.
Kardinali alisema , nasi licha ya mahali tupo na tulivyo, tunaitwa kuteremka hima kutoka katika starehe za dhambi na kukutana na Yesu, anayetaka kula chakula pamoja nasi katika mioyo yetu, nyumba zetu na familia zetu.
Kardinali aliendelea kusema, Yesu, aliwapokea wote kama ndugu , wema wenye dhambi, wanafiki na watoza ushuru. Mwinjilisti Luka , kwa kweli, anatoa changamoto kwetu, kuvunja kuta za utengano kati ya wale wanaofikiri ni wema na wale wenye dhambi.
Na kwamba huu ni mwaliko kwa wote wanaofika katika madhabahu hayo, ili kwamba, tokea hapo, wote wawe wamemeitikia mwaliko wa kushirikiana na umoja watu wote kama mawe hai ya msingi, yakiinua moja kwa jingine, kusaidia kuidumisha nyumba ya Mungu yaani Kanisa, na ujenzi wa misingi ya maisha ya Kikristu kwa watu wote. Aliongeza, kwamba, hata katika hali za umasikini, kanisa linapaswa kuendelea na utume huu wa kuishi kwa upendo na shikamano, na hasa katika kuihubiri habari njema kwa watu wote, matajiri, maskini na wanyonge.
Kardinali Tarcisio, akihitimisha maadhimisho ya Siku Kuu ya Mama Yetu wa Fatima, pia alitaja jinsi maisha yetu yanavyoishi katika hali za vitisho na udhaifu na hatari nyingine zinazo jitokeza katika uzoefu wa maisha ya kutokuwa na uwezo wa kuyatawala ya usoni tusiyoyajua, hofu kwa madhulumu na maut. Lakini akasisitiza kwamba, tuna neno la mwisho juu ya uwepo wa binadamu, ambalo ni matumaini ya kweli katika kupata ushindi juu ya dhambi na mauti na changamoto za maisha. Neno lenye kutoa ujasiri na maamuzi ya kutaka kuuona uso wa Mungu, katika maisha yetu. Neno la Injili ya kuokoa inayongoza katika maisha ya milele yasiyokuwa na wasiwasi na hofu.

Kardinali alitaja kiini cha ujumbe wa Tukio la Mama Yetu Fatima kwamba , ni uongofu kwa Mungu, kanuni inayorejesha upya jamii ya binadamu wote kwa Mungu. Matukio ya Maria kuwatokea kwa mara kadhaa watoto wa Fatima, ni mwaliko unao tutaka tujibidishe katika juhudi za kutaka kuuona uso wa Yesu. Ubinadamu wetu wote ni pamoja na Maria, katika uhakika kwamba, upendo huamini yote, hutumaini yote, hustahimili yote, alieleza Kardinali Tarcisio. Kama sisi tunaishi katika umoja na Mungu , kwa njia ya Maria hofu huteketea, kama mandhari ya kichungaji iliyoandikwa katika madhabahu hayo inavyosema : " Usiogope ".








All the contents on this site are copyrighted ©.