2013-10-14 15:04:06

Wakristu ,igeni maisha ya wafia dini-Papa Francisko


Papa Francisko ametoa wito kwa Wakristu, kuwaiga mashahidi wafia dini ili kuondokana na hali ya kuwa wakristu bandia.
Papa alitoa wito huo, siku ya Jumapili, kwa njia ya video , katika ujumbe wake, kwa ajili ya tukio la kihistoria la kutajwa kuwa Wenye Heri, mashahidi wafia dini 522 , Wahispania, waliouawa wakati wa adha ya mapambano dhidi ya Ukristo katika ya miaka ya 1930.

Katika ujumbe huu, Papa ameonyesha ukaribu wake katika sherehe hizi zilizofanyika Tarragona, Hispania , ambako idadi kubwa ya Mapadre, ,na watawa, na walei aminifu katika imani , walitangazwa kuwa Wenye Heri Mashahidi wa Imani, Jumapili iliyopita. .

Hotuba hiyo fupi ya Papa kwa ajili ya tukio hilo, amewatazama kwa makini sana, mashahidi hao na kusema kwamba, hawa walikuwa ni Wakristo wa kawaida, lakini waliishi kwa uaminifu, katika kuifuata njia ya Kristo. Ni wanafunzi wa Yesu waliojifunza vyema anachokitaka Bwana wao, kwamba ni upendo wa hali ya juu kwa Kristu, kama Yeye Yesu alivyotembea katika njia hiyo hadi mauti msalabani kwa ajili ya utukufu wake Mungu.

Papa akiuelezea upendo huo anasema, haukuwa upendo nusunusu, au uliotolewa kwa vipindivipindi bali ni ulikuwa ni upendo kamili. Ni upendo unaokwenda hadi miisho ya maisha, juu ya msalaba. Pamoja na Yesu kuusikia uzito wa mauti , uzito wa dhambi za binadamu, hakusita kuitoa nafsi yake nzima kwa Baba, kwa ajili ya kumkomboa binadamu, na mzigo huo wa dhambi. Akiwa msalabani Yesu alitoa maneno machache, lakini muhimu, yaliyo toa zawadi ya maisha. hili linaonyesha wazi kwamba, Kristo anatupenda kwa upendo usiokuwa na kiasi. Na ndivyo wafuasi wake Mashahidi wafia dini waliotajwa kuwa Wenye Heri, waliuishi upendo huo mpaka mwisho wa maisha yao.

Papa alihimiza waamini kuyaiga maisha ya wafiadini hawa. Na kwamba ni lazima daima kufa kwa ajili ya kujitakatifusha wenyewe, dhidi ya binafsi wetu, ustawi , uvivu wetu, majonzi yetu, na kujifunua kwa Mungu,na kwa wengine , hasa wale wanao tuhitaji zaidi.

Papa aliendelea kuomba maombezi ya mashahidi, ili tuwe Wakristo halisi wa kweli, Wakristo katika matendo na si tu kwa maneno , tusiwe Wakristu vigeugeu lakini thabiti katika upendo wa hali ya juu kwa usiokuwa butu, hadi mwisho wa maisha. Papa aliomba msaada wao katika kudumisha imani yetu thabiti , hata wakati wa matatizo yetu, na katika kuboresha matumaini na kukuza udugu na mshikamano.








All the contents on this site are copyrighted ©.