2013-10-14 12:01:58

Siku kuu ya Mama Yetu wa Fatima: Papa ahimiza waamini kusema "ndiyo" kama Maria.


Jumapili iliyopita 13 Oktoba, ambayo ilikuwa ni Sherehe ya maadhimisho ya Siku Kuu Mama Yetu Maria wa Fatima , tukio lililoandaliwa kama sehemu ya maadhimisho ya Mwaka wa Imani, kwenye kumbukumbuku ya Bikira Maria kuwatokea watoto wa Fatima 13 Oktoba 1917, Sanamu asilia ya Fatima ililetwa Vatican, na kuwekwa katika Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, mapema asubuhi kwa ajili ya maadhimisho ya Ibada ya Misa iliyoongozwa na Papa Francisko.
Mara baada ya Ibada, Papa pia, aliiweka wakfu dunia kwa Moyo Safi wa Maria, Ibada hii ya Misa iliyohudhuriwa na umati wa watu zaidi ya laki moja, katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtaktifu Petro. .

Papa Francisko, akiongoza Ibada katika uwanja huo, kwenye homilia yake alitaja mambo matatu: Maajabu ya Mungu, uaminifu kwa Mungu na Mungu ni nguvu yetu."
Papa alizungumzia juu ya kweli hizi tatu, na kuomba msaada wa Maria Mkingiwa dhambi ya asili uzidi kutuongoza katika maisha yetu ya kila siku. Lakini ili tuweze kupata mafao ya msaada huu, Papa alisema muumini anahitaji kuwa na maisha adilifu na aminifu katika imani, kutolea shukurani na sifa Mungu na kumtukuza Kristu aliye nguvu yetu.
Papa alieleza kwa kuirejea Zaburi :” Mwimbieni Bwana wimbo mpya , kwa maana ametenda mambo ya ajabu" ( Zab 98:1 ). Papa alifafanua leo tunaona moja ya mambo ya ajabu ambayo Bwana amefanya : Maria ! Kiumbe wa hali ya chini na dhaifu kama sisi wenyewe, lakini yeye alichaguliwa kuwa Mama wa Mungu , Mama wa Muumba wake.

Papa aliendelea kumtaza Maria kwa makini , na kutoa mwaliko kwa waumini kutafakari kweli hizo tatu , kulingana na neno lake( Lk 1:38 ), ambamo tunaona kuwa utendaji wa Mungu daima hushangaza, kwa kuwa katika kupungukiwa , udhaifu na fedhaha ndimo hujionyesha upendo wake wa kutuokoa kutuponya na kutupatia nguvu. Na anachokiomba ni tu kulitii neno lake na kumwamini.
Na hayo ndiyo maisha aliyo yaishi Bikira Maria . Wakati akipata ujumbe wa Mungu toka kwa Malakia hakuweza kuficha mshangao wake .Alishangaa kwa jinsi Mungu anaweza kuwa binadamu , kuptia kwake, yeye aliyekuwa binti maskini wa Nazareth. Mungu hakuchagua binti anayeishi katika majengo ya kifahari na mwenye mamlaka au utajiri mkubwa, wala aliyekuwa ametenda mambo makubwa ya kushangaza , lakini anamchangua Maria, anayeishi maisha ya kawaida ambaye moyo wake umejifunua kwa Mungu kwa unyenyekevu na utii. Maria baada ya kupaswa habari na Malaika , bila ya kuelewa vyema kila kitu alisema ndiyo kwa mungu , mimi hapa Mtumishi wake , nitendewe kana unavyonena.
Papa anasema, kwa wengi wetu, kuna ugumu kubaki imara na aminifu katika maamuzi tunayofanya na ahadi tunazo weka. Mara nyingi ni rahisi kusema "ndiyo" , lakini tunashindwa kurudia "ndiyo" kila siku. Tunashindwa kuwa waminifu.

Maria akasema "ndiyo yake" kwa Mungu: " ndiyo" ambayo ilibadilisha maisha yake. Ndiyo aliyoitaja hata wakati wa uchungu na huzuni kuu. Ndiyo katika kilele cha maisha ya mwanae chini ya Msalaba. Mwanamke mwaminifu , bado amesimama , chini ya msalaba akiwa amevunjika moyo lakini bado mwaminifu na mwenye nguvu.

Papa alieleza na kuhoji iwapo sisi kama Wakristu tuna ndiyo hiyo ya kuishi na Mungu nyakati zote katika furaha, uchungu, mateso na hata mauti. Mungu anatutaka kuwa waaminifu kwake, kila siku katika maisha yetu ya kila siku . Huruma ya Mungu kamwe haiachi kuuonyosha mkono wake wa kutuinua sisi juu, kututia nguvu katika safari yetu, na kutembea pamoja nasi licha ya udhaifu wetu, ili aweze kutupatia nguvu zake. Hii ni safari halisi: kutembea na Bwana siku zote , hata katika wakati wa udhaifu , hata katika dhambi zetu.
Papa alieleza na kuhimiza waamini kung’ang’ana na jibu la ndiyo, katika kumfuata Yesu, ahadi waliotoa wakati wa ubatizo. Ni kuzikataa njia zote zinazotaka kutupeleka nje ya njia ya Yesu, ambazo huua mwili na Roho. Ni kubaki na jibu la ndiyo , kama ilivyokuwa kwa Maria.

Papa akizungumzia Mungu ni nguvu yetu . Aliwatazama kwa makini ,watu kumi wenye ukoma walioponywa na Yesu katika Injili, waliosimama mbali nae na kuita kwa sauti kuu, Yesu Mwalimu, utuhurumie ! (Lk 17:13). Yesu aliwaangalia wagonjwa hao kwa huruma, aliona wanahitaji upendo na nguvu. Walihitaji kupona, na Yesu kwa upendo na huruma yake akawaponya. Lakini baada ya kuponywa ni mmoja tu aliyerudi nyuma kutoa asante na kumtukuza Mungu. Yesu anauliza wengine wamekwenda wapi, mbona ni mmoja tu aliyerudi na kushukuru na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa na kukiri kwamba yeye ndiye mwenye nguvu iliyomponya?. Papa anasema, hili ni fundisho kubwa kwa wamini. Alibaini, tunafahamishwa kwamba, ni muhimu kutoa shukrani , kutoa sifa kwa ajili ya kila kitu Bwana amefanya kwa ajili yetu .

Papa alieleza na kumrejea tena Maria ambaye baada ya kupashwa habari kwamba atamzaa Yesu, Masiya Mkombozi wa dunia ,tendo lake la kwanza ni tendo la upendo, kwenda kumtembelea jamaa yake Elizabeth mzee. Na Maneno yake ya kwanza, ilikuwa " Moyo wangu wamtukuza Bwana ", kwa maneno mengine, huu ni wimbo wa sifa na shukrani kwa Mungu si tu kwa kwamba alifanya kwa ajili yake, lakini kwa yale aliyoyatenda katika historia ya wokovu. Kila jambo na kila kitu ni zawadi toka kwa Mungu .
Kama tunaweza kutambua kwamba kila kitu ni zawadi ya Mungu , jinsi gani ilivyo furaha kwa mioyo yetu! Kila jambo na kila kitu ni zawadi yake . Yeye ni nguvu yetu! Papa alifundisha na kutahadharisha kusema " asante" ni jambo kama rahisi, na hivyo bado ngumu! Mara ngapi sisi tunasema asante mmoja kwa mwingine katika familia zetu? Haya ni maneno muhimu kwa maisha yetu ya kawaida. Mara ngapi sisi ni kusema asante kwa wale wanao tusaidia au walio karibu nasi, na wale walio tuunga mkono katika maisha yetu?.
Papa anaonya mara nyingi kuna mwelekeo wa kujisahau na kuona kupewa kitu au kutendewa mema ni haki yetu . Anasema sawa ni haki yetu lakini pia ni wajibu na tunapaswa kusema asante kwa kila jambo ! Asante kwa Mungu . Ni rahisi kwa njia ya sala kumwomba Bwana mahitaji yetu, lakini, tazama jinsi ilivyo rahisi mara tunapojaliwa, kusahau kwenda na kushukuru. Tunaona hakuna haja, hatuma muda. wakati wa kuomba tulikuwa na muda, lakini muda huo haupo wakti wa kushukuru ! Papa aliasa na kuhitimisha kwa kuomba msaada wa maombezi ya Maria, atusaidie kuyaona matendo ya kushangaza ya Mungu , kuwa waaminifu kwake na kila siku, kumsifu na kumshukuru , kwa kuwa yeye ni nguvu yetu.








All the contents on this site are copyrighted ©.