2013-10-09 08:05:48

Msijifungue majumbani bali tokeni mkakutane wa watu-CCEE


Maaskofu wa Ulaya waambiwa "msijifungie katika ngome zenu,tokeni nje mkakutane na watu kama viongozi wa matumaini". Ni jibu la Kanisa la Ulaya katika kufanya mageuzi kwenye mamlaka ya Ulaya. Bila kujali nini kinatokea, wakristu wamehimizwa kudumisha utambulisho wao wazi uliosimikwa katika imani kwamba, imani yao ni hai nyenye kuvuvia daima mwamko wa tumaini jipya.

Matumaini, ni neno lililo hitimisha Mkutano wa Marais wa Mabaraza Katoliki Ulaya, (CCEE) Jumapili iliyopita huko Bratislava, Slovakia. Katika siku hizo za mkutano, Maaskofu wameweza kujadili mada “Mungu na serikali , Ulaya kati ya watu na Malimwengu", na changamoto katika kuwasilisha tamko la mwisho iliyotolewa Jumatatu na CCEE. Majadiliano yao yalifuatiwa na mada ya utafiti, mara kadhaa kwa ajili ya kuimarisha tumaini, imani na uzoefu na maudhui ya kuvutia kwa kila mtu.

Mara kadhaa , Maaskofu walikiri kwamaba imani katika matumaini, huliwezesha kanisa kudumu duniani. NI tumaini linalowapa Wakristo, ujasiri wa kukabiliana na hali ngumu na roho ya uwazi kwa hoja za watu, zaidi ya yote kwanza kabisa ni utume wa uinjilishaji wa kanisa.
Inaendelea CCEE –ni lazima kuwa tayari wakati wote kuingilia kati katika maamuzi muhimu yanayotolewa na serikali na hivyo Kanisa sio kubaki tu katika kufikiria mambo ya kiroho.
Mkutano huo pia ulifanya uchambuzi kwa jinsi gani wanaweza kukabiliana na hali halisi za kijamaa na kupendekeza mbinu chanya na utendaji kuelekea hali halisi na mienendo ya kijamii.Na pia walitazama suala la wakimbizi wanaowasili na kusisitiza haja ya kujenga mshikamano wa mataifa ya Ulaya kwa ajili ya kukabiliana na hali hii kama ilivyojitokeza siku hizi katika kisiwa cha Lampedusa, ili isijirudie tena na pia walijadili na mgogoro wa kiuchumi, na kutoa jibu linalohimiza wenye navyo kuwagawia wasiokuwa navyo, watu masikini, kama Papa Francisko alivyo himiza wakati akitembelea kituo cha Lampedusa, na katika homilia zake kadhaa.







All the contents on this site are copyrighted ©.