2013-10-07 15:28:08

Waathirika wa Lampedusa wakumbukwa Vatican kwa ukimya na maombi.


Jumapili, Papa Francisko, aliwakumbuka kafara na waathirika wote wa Lampedusa, kwa kukaa kimya kwa muda wa dakika chache wakati wa sala ya Malaika wa Bwana, aliyosali mbele ya maelfu ya mahujaji na wageni , waliofika kusali pamoja katika uwanja wa kanisa kuu la Mtakatifu Petro.

Zaidi ya watu mia wamethibitishwa kufa maji baada ya boti waliokuwa wakisafiria kushika moto, kabla ya kufika katika bandari ya kisiwa cha Lamepdusa, Alhamis iliyopita. Wengi wa wasafiri hao wenye asili ya Afrika, walikuwa wakijaribu kuingia Ulaya bila kibali na kwa njia isiyo halali.

Baada ya ukimya huo, Papa alihutubia umati wa watu waliokusanyika katika Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro. Na hotuba yake ilianza kwa kurejea, ziara yake ya Kichungaji Assis, ambako pamoja na nia ya kwenda kusali, mahali alipoishi wajina wake Mtakatifu Francis,na kukutana na watu wa Assis pia ilikuwa na nia ya kushiriki katika maadhimisho ya Sikukuu ya Mtakatifu Francis, Oktoba 4. Papa alitrudia kutoa shukrani zake za dhati, kwa makaribisho mazuri, waliyo mpatia watu wa Assis.

Na akitafakari Somo la Injili ya siku , Papa alizungumzia nguvu ya imani , huku akitoa mwaliko kwa umati uliokuwa ukimsikiliza, kurudia kwa mara kadhaa , ombi alilolitoa “Bwana, tuongezee imani yetu”. Na aliwazungumzia wale ambao ni wepesi wa moyo na wanyenyekevu , au wale wanao yapokea matatizo katika maisha yao kwa moyo wa unyenyekevu na kuyakubali matatizo kama sehemu ya maisha yao, ambao hujiona si kitu mbele ya Mungu na jirani , ingawa wana uwezo wa kufanya mambo makubwa, wenye kudumisha utulivu fulani, kwa sababu ya imani yao.

Aidha Papa Francisko, alikumbusha Mwezi wa Oktoba, ni mwezi uliotengwa rasmi kwa ajili na majitoleo ya namna ya kipekee kwa wamisionari , hasa wale ambao wanapambana na vikwazo vigumu katika kuitangaza Injili. Alisema, uwepo wao ni fundisho kwa Wakristu wote kwamba, kila mmoja katika maisha yake mwenyewe ya kila siku, ni wakati wa kumshuhudia Kristo , kwa nguvu ya Mungu, nguvu ya imani.

Papa alisema“Nguvu hii hupatikana kupitia maombi. Maombi ni pumzi ya imani. Katika uhusiano ambapo kuna imani na upendo, aliendelea, kuna haja ya kuwa na mazungumzano. Maombi ni mazungumzo kati ya nafsi ya mtu na Mungu”.

Aidha Baba Mtakatifu alikumbusha pia, Oktoba ni mwezi wa Rozari ,kama ilivyo katika Kalenda ya Liturujia, ikianza na Jumapili ya kwanza ya mwezi huu. Kumwomba Mama Yetu wa Pompei , Mbarikiwa Bikira Maria wa Rosari Takatifu. Papa Francisko ameeita Ibada ya Rozari, kuwa ni "shule ya sala ," na " shule ya imani! "

Na baada ya sala la Malaika wa Bwana, Papa alizungumzia Rolando Rivi , mseminaristi mwenye miaka 14, shahidi wa imani, aliyeuwa mwaka 1945, ambaye alitangazwa Mwenye Heri Jumamosi iliyopita, huko Modena Italy .
Papa alisema jinsi gani kijana huyu ni mfano mkubwa kwa vijana wa leo . "Yeye alijua ambapo alikuwa na kwenda ... alijua upendo wa Yesu katika moyo wake, na alitoa maisha yake kwa ajili upendo huo wa Yesu.
Papa Francis alihitimisha tukio hili la Sala ya Malaika Bwana kwa kumtakia kila mmoja Jumapili njema.








All the contents on this site are copyrighted ©.