ni nini kilichofichika katika mashambulio ya tindikali Zanzibar ?
Serikali ya Tanzania imehimizwa kutotegemea tu jeshi la polisi kupambana na mashambulio
yanayofanywa dhidi ya watu mbalimbali Zanzibar, bali itafute mbinu nyingine mpya
ya kuwanasa wahalifu hao, kwa mfano kuunda tume maalum kwa ajili hiyo. Mhariri wa
gazeti la The Guardian Tanzania, ameishauri serikali kufuatia shambulio baya la kumwagiwa
tindikali Padre Mkatoliki Ijumaa iliyopita, ukiwa umepita mwezi mmoja tu tangu kulipo
fanyika shambulio jingine kama hilo, kwa wasichana wawili wa Uingereza kumwangiwa
tindikali na wtu wasiojulikana.
Mpaka sasa hakuna mtu au kundi linalodai kuhusika
na mashambulio hayo wala kutajwa lengo na nia za vitendo hivyo viovu vilivyo nje
ya ubinadamu.
Mhariri wa The Guardian katika tahariri yake ya Jumapili alisema,
wao mpaka sasa hawana vithibitisho kama mashambulio haya ni kwa sababu za kidini ,
lakini ni wazi mazingira ya mashambulio yanayonyesha ni vikundi vya wababe wasiovumilia
wenigne. Na cha kusitisha zaidi, mpaka sasa hakuna waliokwisha kamatwa kuhusika na
matukio licha ya polisi kuahidi donge nono la fedha, kwa atayeisadia polisi kuwanasa
watu hao. Kutokamatwa kwa wahalifu kunatia wasiwasi kama kweli polisi iko makini katika
kuwatia mbaroni wahalifu hao.
Katika mazingira hayo, Mhariri wa The Guardinai
Jumapili alitoa ombi lake kwa serikali kuunda tume maalum wakiwemo watalaam kutoka
idara mbalimbali kwa ajili ya kupata kiini cha sababu ya mashambulio hayo Zanzibar.
Rais wa Zanzibar , Dr Mohammed Shein, Jumapili aliiagiza Idara yapolisi katiak
visiwa hivyo kufanya upelelezi w akina ju ya mashambulio haya ya kutumia tindikali
na wahalifu wakamatwe na kufikisha mbeleya sheria mara moja. Dr Shein alitoa agizo
hilo, Jumapili wakai akimtembelea Padre Anselmo Mwangamba wa Kanisa Katoliki, aliyemwangiwa
tindikali na watu wasiojulikana na kwa wakati huu amelazwa ktiak hospitali ya mnazimmoja
mjni Zanzibar.
Dr Shein alisema , shambulio kama hili ni unyama wa hali ya
juu unaoweza kufanyika tiak jamii iliyodtaraabika , na hivyo serikali yake haiwezi
kuwavumilia wahalifu kama hao , na polisi ni lazima wafanye kila jitihada kuwapata
wahalifu hao. Na akizungumza na baadhi ya Wakatoliki waliofika hospitalini kumjulia
hali Padre Alnselm , Dr Shein aliwataka wawe na uvumilivu , na serikali itahakikisha
wahalifu wnatiwa mbaroni.
Nalo gazeti la This Day limetaarifu kwamba, baadaye
Padre Anselmo, ambaye asilimia 30 ya mwili wake umeathiriwa na tindikali, hasa sehemu
za usoni , alihamishiwa katika Hospitali ya Kitaifa ya Rufaa ya Muhimbili Dar-es
Salaam na kwamba kwa bahati macho yake hayakudhurika . Padre Anselmo amelazwa katika
wodi ya wagonjwa ya Kibasila, kwa matibabu zaidi.