2013-09-14 15:22:47

Papa ahimiza imani katika uwezo wa kuokoa wa Msalaba


Ijumaa , Baba Mtakatifu Francisko aliwapokea na kuwahutubia wajumbe kutoka Jumuiya ya ulinzi wa Kaburi Takatifu la Jerusalem , ambao wako Roma kwa ajili ya Mkutano wao wa Mashauriano. Jumuiiya hii ya tangu karne za kale, ina kanuni ya kuwa na mkutano wake mkuu kila baada ya miaka mitano,kwa lengo la kutafakari kwa kina nia za jumuiya na hali ya jumuiya Katoliki katika Nchi Takatifu , na kutathimini zake juhudi mbalimbali katika utendaji wa Jumuiya , hasa masuala yanayohusiana na utawala, mamlaka na mipango kwa siku za mbele .
Baba Mtakatifu akizungumza na washiriki wa mkutano huu, mjini Vatican, alilenga zaidi nguzo tatu za maisha ya Mkristu, kuwa ni, kusafiri , kujenga na kukiri imani, ambayo yamekuwa msingi wa mafundisho ya utawala wake tangu alipochaguliwa kuwa Papa na Makardinali wenzake miezi sita iliyopita.
Papa aliwaambia safari yenu , iko katika historia ya dunia ambayo mipaka yake daima hupanuka na vikwazo vingi kuanguka na mapito yenu daima yakifungamana zaidi na zaidi katika upendo wa mmoja kwa mwingine. Na hivyo aliwahimiza Wanajumuiya wa Ulinzi katika Kaburi Takatifu, kuziishi karama na mapokea ya utamaduni wao kwa uaminifu, unyenyekevu na upendo katika huduma ya kujenga yaliyo bora zaidi kwa siku za usoni , na kwa ajili ya mshikamano na Wakristu wa Nchi Takatifu katika mapambano yanayowakabili.
Papa aliendelea kuwaasa kwamba, mwendo wao katika kumfuasa Kristu ni lazima uchipuke ndani na kukua ndani ya mioyo yao kwa kuikiri imani kwa uaminifu zaidi , na kukua katika juhdui zote zinazolenga kuilisha roho ya maisha ya imani, aliyechipushwa na majiundo ya muda mrefu ya roho wa Kikristu katika umoja na mshikamano wa kweli wa maisha na Kikrstu.
Aidha kuamini kaiak uwezo wa Msalaba na ufufuko wa Bwana , Papa alisema, ni kujenga tumaini na amani katiak maisha. Na namna ya pekeee Nchi ya Yesu inahitaji uwepo wao zaidi na zaidi. Papa aliwataka wasijitenge mbali na uwajibikaji , bali daima imani na iwe kichocheo na msukumo wa kuwajenga imara zaidi katika utendaji wa kazi katika tumaini la kuwa na jamii iliyo bora zaidi.








All the contents on this site are copyrighted ©.