2013-09-12 14:42:58

Tazama ilivyo vyema kuwapenda wengine - Ujumbe wa Papa wa mapema Alhamis


Mapema Alhamis hii, Mama kanisa akiadhimisha Siku Kuu ya Jina Takatifu Sana la Maria, Baba Mtakatifu Francisko aliongoza Ibada ya Misa katika kanisa dogo la Mtakatifu Martha hapa Vatican, ambamo katika homilia yake alisema, Wala hatuhitaji kuhoji mengi juu ya uzuri wa Siku Kuu ya leo kwani hakuna asiyeutambua uzuri wa Jina Takatifu Sana la Maria. Wema wa Mama Bikira Maria, hutufanya sote kuelewa mafundisho mengi ya Yesu, katika namna tunazopaswa kuyaishi.

Papa aliasa pengine inaweza kuonekana ni maisha yenye orodha ndefu na ngumu kuiishi, kama ilivyo amri kuu, Mpende adui yako na mtendee mema , na yule anayekupiga kofi shavu moja mpe na la pili , na yule anataka kuchukua joho lako mpe na kazu pia. , Ni maneno mazito haya , Papa alisema . Lakini yote haya kwa namna zake mbalimbali, Bikira Maria Mtakatifu, aliuishi ukweli huo , Mama aliye neema ya yote na neema ya unyenyekevu, jina linalong'ara kuliko majina yote, Maria nyota ya asubuhi inayowaangazia na kuwaongoza wafuasi wote wa mwanae kuuishi upendo wa kweli wa Mungu.

Papa aliendelea kusema, "tunaweza kutafakari na kuelewa mafundisho ya Yesu , iwapo mioyo yetu, na iwapo nia yetu ni pamoja na Yesu, mshindi, aliyetushindia mauti, dhambi na dhidi ya utendaji wote wa shetani, na ili nasi kama waamini wake, tuweze kutenda kama Yesu anavyotutaka. Na hili linahitaji si mengine kama Mtume Paulo alivyosema: ni kuishi maisha ya upole, unyenyekevu, wema, huruma,na bila ya kujikuza. Kama hatukazi nyuso zetu katika kumtazama Yesu , basi hatuko pamoja na Yesu, na hatuwezi kutenda kama anavyotaka. Kuwa na Yesu ni neema, ni neema inayotokana katika kutafakari sana sura ya Yesu".


Papa alieleza na kushauri kwamba , inafaa kutenga muda wa ukimya na kufikiri kwa makini juu ya Yesu, na kw akufanya hivyo tunapata nguvu ya kuwa nae. Yeye mwenye aliye uweza wote, huayatimisha pia yale yaliyotupungukia. Lakini ili kupata neema hii , tunapasea kuyaweka maisha yetu yote kwa Mungu kupitia Kristu .Ni kuitafakati sura halisi ya Yesu aliye mwilishwa na kukaa kwetu katika hali ya ubindamu, akiyaishi maisha yote ya furaha na mateso. ili tuwweze kufanana nae hatuja njia nyingine, ni kuyapita mapito yake kama ilivyokuwa kw Mtakatifu Sana Bikira Maria Mama yake alivyoziishi siku za furaha huzuni na kutukuka kwake baada ya kifo na madhulumu ya binadamu. Vivyo hivyo, kwa mfuasiw a kweli wa Yesu hakuna njia nyingine ili kuishi na kutembea pamoja katika hali zote.

Ili tuweze kuwa Wakaristu wazuri, tunapaswa kuutafakari umwilisho wa Yesu tukilinganisha na ubindamu wa wa watu wateswa, kwa ajlli ya shuhuda kwa watu wote, tukisamehe na kumtafakari Yesu Mteswa, anayeonekana katiak sura ya jirani anayeteseka. Ni kuyaficha maisha yetu katika maisha na madonda ya Yesu Kristu , Mungu aliyejishusha, kama anavyotushautri Mtume Paulo , ni katika kutenda kwa wema, unyenyekevu,upole, ukarimu na saburi.










All the contents on this site are copyrighted ©.