2013-09-09 09:08:07

Vita ya Syria, vinakuzwa na soko la biashara haramu ya Silaha


Vita ya Syria ni vita vya biashara haramu ya silaha, isiyojua ubinadamu.
Baba Mtakatifu Francisco, Jumapili wakati wa sala ya Malaika wa Bwana, aliendelea kutoa wito wa amani kwa dunia , kupitia mafuriko ya watu waliokuwa wamekusanyika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro Vatican. Alisema na tuendelee kusali na kutenda kwa ajili ya kufanikisha amani , na hasa kusitisha ukatili wote wa kivita unaofanyika Syria.
Papa alirudia kutoa ombi lake akiwa bado amemezwa na mvuto wa mafungo na mkesha wa sala wa Jumamosi , aliyo ongoza kwa ajili ya kuombea amani Syria, Mashariki ya kati na duniani kote. Ilikuwa hasa kuhamasisha usitishaji wa vita vya wenyewe kwa wenyewe katika taifa la Syria, ambavyo kwa sasa vimeingizwa katika mtengo wa biashara haramu ya silaha.

Papa Francisko aliendelea kutafakari picha ya amani duniani, akisema kwa hakika amani imetiwa uvuli na nia binafsi, zenye wivu na chuki, ubinafsi unaorarua moyo wa udugu na urafiki. Matokeo yake ni utendaji mbovu dhidi ya maisha ya watu na ubinadamu , kama ilivyo sasa Syria na Mashariki ya kati. Mgogoro wa kisiasa umeingia katika mtengo wa mfumowa mashindano ya biashara haramu ya silaha.

Hii ni hatari kubwa na watu wote ni lazima wasema hapana. Hapana kwa choyo, wivu, chuki, majivuno na na vinyongo na utengano , kwa kuwa havisaidii kitu, bali ni uvurugaji tu, wa amani na utulivuna ustawi wa jamii. Ni kujinasua katika mtego huu wa biashara haramu ya silaha.

Papa kwa nguvu zote alipaza sauti yake akisema, Sasa chuki basi kati ya watu . Sasa basi, kwa vita inayopiganywa kumbe ndani mwake , mmefichika nia na malengo binafsi, yasiyokuwa na manufaa kwa jamii . Huu wa wakati wakuskiliza kilio cha watu wenye mapenzi mema, waliozama katika mafungo na sala, kuombea amani Syria.

Papa alihoji, katika mtazamo wa kina, vita inasaidia nini ? Kama tu siyo kuleta ghasia na kuivuruga jamii ? hakuna vita yenye kuletea mema jamii na hasa katika ulimwengu wa sasa, ambamo wengi wanasubiri kwa hamu nafasi ya kuuza silaha zao walizozalisha kwa wingi lakini hawana tena soko la kuuza silaha hizo. Hivyo ni lazima jamii iwe macho kwamba, machafuko kidogo ya jamii kudai haki , inakuwa ni nafasi kwa wafanyabashara ya silaha kujipenyeza na kukuza machafuko hayo, ili waweze kuuza silaha zao.
Baba Mtakatifu aliendelea kuasa kwamba, kuna mambo mengi mabaya yanayoletwa na biashara haramu ya silaha. Na daima utendaji wa biashara haramu ya silaha, huzua vita kwa ajili ya kupatikana kwa soko la kuuza silaha. Alieleza soko hili, sababu halisi ya jumuiya ya kimataifa, kupigana nayo, tena kwa mshikamano na umoja thabiti, bila ya kutafuta faida binafsi , bali kwa ajili ya amani na mema kwa watu wote.

Kwa maelezo hayo, Baba Mtakatifu alimalizia hotuba yake na wito wa kusitishwa mara moja ghasia zinazo mwangamiza binadamu, na mali Syria, na Misri. Na tusali ili kwamba Misiri Wakristu na Waislamu , wajiingize kawtiak utendaji wa kujemba amani na mapatano ya kitaifa kwa ajili ya manufaa yao wote. Ni wazi njia ya kufikia manai kamaili na mapatano ni defu yeny kuhitaji uvumilivu, hekima na busara . Pia ameitaka jumuiya ya kimataifa kufanya kazi na majitolea mapya kwa ajili ya ufumbuzi wa mgogoro wa mgawanyiko ulio rarua raia wa Syria, na kwingineko duniani.


"Natuendelee kusali bila ukomo, kuomba amani na utulivu duniani.

Baba Mtaktifu mwanzoni mwa hotuba yake, alirejea tukio la kutangazwa kuwa Mwenye Heri , Mtumishi wa Mungu Maria Bolognesi, ambaye aliyatolea maisha yake yote katika kuhudumia wengine na hasa masikini na wagonjwa . Aliyeweza kushiriki ktiak mateso ya wengine katika kina cha mateso ya Yesu Mfufuka.

Papa alitolea shukurani zake za kwa Mungu kwa ajili ya shahidi huyu wa Injili, Mwenye Heri Maria Bolognesi. .







All the contents on this site are copyrighted ©.