2013-09-05 11:26:35

Papa kuwa na ziara ya Kichungaji Assisi Italy


Baba Mtakatifu Francisko atafanya hija ya Kichungaji kwenye mji asili wa Mtakatifu Francisko wa Assisi wakati wa maadhimisho ya Sikukuu ya Mtakatifu Francisko hapo tarehe 4 Octoba mwaka 2013. Papa alilichagua jina la Mtakatifu huyu alipoteuliwa kuwa Khalifa wa Mtakatifu Petro hapo tarehe 19 Machi mwaka 2012.

Atakapowasili Assisi baba Mtakatifu atapokelewa na Askofu Mkuu wa Assisi, Mons. Domenico Sorrentino na wawakilishi kadhaa wa serikali ya Italia. Baadhi ya shughuli za kichungaji atakazokamilisha akiwa Assisi ni pamoja na kukitembelea kituo cha watoto walemavu cha Serafico na kile cha watu maskini cha Mtakatifu Francisko ambapo atakutana maskini wanaosaidiwa na shirika la misaada la kanisa Katoliki, Caritas.
Katika hija yake, Papa Francisko ataadhimisha ibada ya Misa Takatifu sehemu mbalimbali, pamoja na kuyatembelea maeneo ya kihistoria ya mji huo kama vile Kanisa la Mtakatifu Damiano ambapo inasemekana ndipo Francisko alipaopata wito wake kwa mara ya Kwanza pale Yesu alipomtokea na kumwuomba aende akamjengee nyumba yake.
Papa atayatembelea pia makanisa makuu ya Mtakatifu Clara na Mtakatifu Rufino, na madhabahu ya Rivotorto pamoja na “jela” chumba alichokuwa anatumia Mtakatifu Francisko kwa sala zake baada ya safari zake za kuihubiri injili huku na huko.
Papa pia atakuwa na mikutano ya hadhara na ya faragha na watu mbalimbali kama inavyo onyesha ratiba ya hija ya Papa Assisi iliyotolewa na Vatikani mwanzoni mwa wiki.








All the contents on this site are copyrighted ©.