Papa awaasa vijana kuwa wajenzi wa mazuri, fadhila na ukweli
Papa Jumatano Papa alikutana na kikundi cha vijana wapatao mia tano wa jimbo la Piacenza
-Bobbio Italia, wakiongozwa na Askofu Gianni Ambrosio wa jimbo la Piacenza. Vijana
walikuwa katika hija ya ya kutembelea kitovu cha kanisa, kama sehemu ya maadhimisho
ya mwaka wa Imani .
Katika hotuba yake, Papa aliwaambia vijana kwamba, wana
hazina ya matumaini katika mioyo yao. Na ni wawasilishaji wa tumani , kwa kuwa wao
ndiyo wanayaishi maisha ya sasa na ni watengenezaji wa hali ya baadaye . Ni watendaji
wakuu wa sanaa ya maisha ya baadaye.
Papa alieleza na kutaja shauku za vijana
wengi kwamba ni uzuri, wema na ukweli. Na kwamba hamu hizo zimeandikwa ndani ya mioyo
yao, na wanapaswa kuzikumbatia wakati wanasonga mbele ya maisha, hasa katika kuyajenga
maisha bora ya baadaye.
Ujana ni wakati wa kuyaishi maisha ya sasa na pia
ni kwa ajili ya kujenga maisha ya baadaye. Na hivyo inakuwa ni changamoto kwao, lakini
kwa ujana una uwezo wa kupambana na kupata ushindi, iwapo hawatazembea na kumwacha
mwovu kuvuruga hamu halisi za moyo. Hivyo ni kuwa na ushupavu na kusonga mbele na
hamu hiyo ya kuyatengeneza maisha mazuri , fadhila na ukweli.
Na hii inamaanisha
ni kupigia kelele dhidi maisha yanayoharibu ustaraabu wa uzuri, fadhila na ukweli.
Ni kwenda kinyume na wimbi la hatari la kupenda malimwengu yenye kuangamiza mwili
na roho pia. HIvyo Papa alihimiza, vijana wasonge mbele kwa kutamani mazuri, mema
na ukweli.
Askofu Gianni Ambrosio wa Jimbo la Piacenza Bobbio, ameonyesha
tumaini lake kwamba, vijana kukutana kwao na Papa wameweza kuchota chochote kwa ajili
ya maisha yao ya Kikristu. Na hivyo anawatazamia watakuwa ni mwanga na chachu katika
kuboresha maisha ya vijana Jimboni Piacenza.
Na aliwaambia vijana kwamba,
tukio la kufanya hija katiak madhabahu ya Mtakatifu Petro na kukutana na Papa katika
hija hii, muhimu kwanza kabisa,inakuwa nimwanga wa kuwaangazia katika njia yao
ya maisha. Ni kupata ufahamu kwamba, maisha yetu humulikiwa na mwanga wa uwepo wa
Kristu Mfufuka ambaye daima huandamana na wale wanaompokea katika mioyo yao na kuishi
nae. Na kwa namna hiyo Kanisa linaendelea kuwepo na kutimiza utume wake wa kuifikisha
habari njema ya upendo wa kuokoa kwa watu wote.