Jumatano hii, 28 Augost, Mama Kanisa akiadhimisha Siku Kuu ya Mtakatifu Augostine,
Mwalimu wa kanisa, mwanzilishi na Baba wa Wa -Augoustini, wanashirika Wa-Augustini
walianza mkutano wao Mkuu wa 184, hapa mjini Roma.
Mkutano unao fanyika kwa
mujibu wa kanuni na taratibu za shirika, ukiongozwa na Makamu Mkuu wa shirika Padre
Michael Di Gregorio.
Madhumuni makuu, ni kuona jinsi wanavyoweza kukuza umoja
na mshikamano zaidi, kwa manufaa ya wanashirika wote. Mshikamano na umoja thabiti
katika maisha ya shirika, unaoweza kuonekana kupitia shuhuda za maisha ya wanashirika,
yenye kuangaziwa na mwanga wa maisha ya kiroho wa Mtakatifu Augostine, mahali popote
walipo.
Na kwamba, Mababa wa Mkutano watachambua kwa kina, uwajibikaji wao
katika kufanikisha manufaa ya wote, kama inavyotamkwa katika katiba ya shirika sura
ya XX1. Aidha Mkutano huu, utafanya uchaguzi wa Kiongozi wake , atakayechukua
nafasi ya Padre Robert F. Prevost, anayemaliza muda wa kuwa mkuu wa shirika kwa mujibu
na kanuni za shirika.
Historia ya shirika la Mtakatifu Augostine inasema
Desemba 16 1243, Papa Innocent IV, alitoa tamko lake rasmi lililozitaka jumuiya ndogondogo
katika mkoa wa Tuscany italia, kuungana na kuwa shirika moja la kidini kwa sheria
na njia ya maisha ya Mtakatifu Augostine. Na hivyo Mwezi March 1244, Shirika lilifanya
mkutano wake mkuu wa kwanza mjini Roma, chini ya maongozi ya Kardinali Richard Annibaldi,
mkutano uliwezesha jumuiya hiyo kuanza kama shirika jipya la Mtakatifu Augostine.