2013-08-28 11:10:15

Jumuiya ya kimataifa yahimizwa kutokalia kimya kilio cha wahanga wa vita Syria


Kwa mara ingine Jumuiya ya kimataifa imehimiza kukisikia kilio cha wahanga wa vita Syria. Ni wito uliotolewa na Askofu Mkuu Mario Zenari, Mjumbe wa Papa Syria
AskofuMkuu Mario Zenari, ametoa himizo hili, kwa kurejea ombi lililotolewa na Papa Francisko, Jumapili iliyopita ambamo aliitaka Jumuiua ya Kimataifa kufanya kila linalowezekana kuisaidia Syria kupata jibu linalofaa kusitisha mzozo wa kisiasa unaoendelea.
Askofu Mkuu Mario anasema, jumuiya ya Kimatiafa inao wajibu wa kutoa jibu katika kipeo hicho, ambacho mpaka sasa kimegharimu maisha ya maelfu ya watu wasiokuw na hatia .
Inasikitisha sana kuoana picha zilizo tolewa na kukisikia kilio cha wadogo wasiokuwa na hatia . Hivyo si haki kwa jumuiya ya kimataifa kujifanya haioni mateso na mahangaiko ya watu wa Syria.
Askofu Mkuu Zenari anasema anatolea sala zake kwa wote wale wenye kuwa na mamlaka katika uwanja wa huu wa kimataifa, na viongozi wote katika ngazi hii ya kimataifa , kutumia busara na hekima kupata jawabu la haraka kukomesha kipeo cha machafuko Syria, kama Papa Francisko alivyotoa ombi lake wakati wa sala ya Malaika wa Bwana, Jumapili iliyopita.








All the contents on this site are copyrighted ©.