Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anabainisha
kwamba, Yesu Kristo ndiye Mlango unaowaelekeza watu kwenye maisha ya uzima wa milele;
mlango ambao uko wazi kwa wote.
Baba Mtakatifu anawaalika waamini na watu
wote wenye mapenzi mema, kumwachia wazi malango ya maisha yao ili aweze kuingia na
hatimaye, kuwasaidia kuondokana na ubinafsi, hali ya kutojali wala kuguswa na mahangaiko
ya wengine, kwa kujifungia katika ubinafsi wao!