2013-08-24 10:22:44

Miaka 67 ya huduma ya Kipadre! Hapa si haba!


Monsinyo Joseph Kyeyune aliyekuwa na umri wa miaka 97 na alikuwa anajiandaa kuadhimisha Miaka 67 ya Upadre, hivi karibuni alifariki dunia na kuzikwa kwenye Makaburi ya Kanisa kuu la Lubaga, katika Ibada iliyoongozwa na Askofu mkuu Cyprian Kizito Lwanga wa Jimbo kuu la Kampala, Uganda.

Askofu mkuu Lwanga amemsifu Marehemu Monsinyo Kyeyune kwa moyo wa sadaka na majitoleo yake kwa ajili ya maisha na utume wa Kanisa nchini Uganda. Alikuwa ni kati ya viongozi mashuhuri wa Kanisa Afrika Mashariki kama vile: Kardinali Emmanuel Wamala, Askofu Adrian Ddungu, Askofu Paul Kalanda pamoja na hayati Kardinali Laurian Rugambwa.

Kilele cha maisha na utume wake wa Kipadre kilikuwa ni katika Mwaka 1996 alipojiunga na Mwenyeheri Yohane Paulo II kusherehekea Jubilee ya Miaka 50 ya Upadre kwa kuungana na Mapadre kutoka sehemu mbali mbali za dunia waliokuwa wamekusanyika mjini Vatican kwa tukio hili muhimu. Hawa ni Mapadre waliokuwa wamepadrishwa kunako Mwaka 1946. Wengi wao katika Jubilee hii waliletwa wakiwa wamebebwa kwenye viti maalum vya wagonjwa!







All the contents on this site are copyrighted ©.