Miaka 35 tangu Mzee Jomo Kenyatta alipofariki dunia!
Askofu msaidizi David Kamau wa Jimbo kuu la Nairobi, anawaalika waamini na wananchi
wa Kenya katika ujumla wao kujenga mshikamano, umoja wa kitaifa, uzalendo na mafao
ya wengi. Askofu msaidizi Kamau ameyasema hayo tarehe 22 Agosti 2013 wakati wa kumbu
kumbu ya siku aliyofariki dunia Mzee Jomo Kenyatta, Rais wa kwanza wa Kenya, yapata
miaka 35 iliyopita.
Enzi ya uhai wake, Mzee Jomo Kenyatta aliwajengea wananchi
wote wa Kenya moyo wa uzalendo na uhuru, mambo ambayo yanapaswa kuendelezwa hata wakati
huu kwa kujikita katika mchakato wa maendeleo ya Kenya. Kama binadamu Mzee Kenyatta
alikuwa na mapungufu yake, lakini aliona ari na moyo wa kutaka kujenga na kuimarisha
nchi ya Kenya kwa ajili ya mafao ya watu wake.
Ni mwaliko kwa waamini na watu
wote wenye mapenzi mema kutoka kifua mbele kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya Kenya.
"Yaliyopita si ndwele wagange ya sasa na yale yanayokuja"! Hayati Mzee Jomo Kenyatta
kunako mwaka 1976 alipata fursa ya kuzungumza na Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya
na kuwataka kuimarisha maadili na utu wema kwa kukemea maovu ndani ya Jamii. Aliwaambia
kwamba, ikiwa kama Jamii itakwenda mrama, viongozi wa kidini watawajibika!
Mzee
Jomo Kenyatta alifariki dunia hapo tarehe 22 Agosti 1978 akiwa Mjini Mombasa.