2013-08-19 15:07:09

Benedikto XVI atembelea Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo


Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita, Jumapili mchana alitembelea kwa muda mfupi Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo. Akiwa mahali hapo, aliweza kusali Rozari pamoja na kusikiliza tamasha la muziki lililokua limeandaliwa kwa heshima yake.

Baadaye jioni, Baba Mtakatifu mstaafu alirejea tena mjini Vatican kuendelea na maisha yake ya sala na tafakari kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya Kanisa la Kristo.







All the contents on this site are copyrighted ©.