2013-08-17 12:01:12

Ajali ya meli yasababisha maafa makubwa nchini Ufilippini


Baba Mtakatifu Francisko amemtumia salam za rambi rambi Askofu mkuu Jose S. Palma wa Jimbo kuu la Cebu nchini Ufilippini kufuatia ajali ya Meli ya Abiria iliyokuwa imebeba abiria 841 na kati yao 600 wameokolewa baada ya Meli ya abiria kugonga na Meli ya mizigo iliyokuwa inaingia bandarini usiku wa kuamkia, Jumamosi, tarehe 17 Agosti 2013. Watu 200 hawajulikani waliko na baadhi ya miili imekwishapatikana.

Ujumbe wa Baba Mtakatifu umeandikwa kwa niaba yake na Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican. Baba Mtakatifu anawaombea abiria wote waliopoteza maisha yao pumziko la milele na kwa majeruhi kupata nafuu ili hatimaye, waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku. Baba Mtakatifu anapenda kuwafariji wote walioguswa na maafa haya kwa njia ya sala na sadaka yake.







All the contents on this site are copyrighted ©.