2013-08-12 11:58:15

Mshikamano na wakimbizi kutoka sehemu mbali mbali za dunia!


Baraza la Maaskofu Katoliki Hispania linaadhimisha Juma la 41 la Wakimbizi na Wahamiaji, ili kutoa msukumo wa pekee kwa Jamii kuangalia na kuguswa na mahangaiko ya wakimbizi na wahamiaji wanaotafuta hifadhi ya maisha Barani Ulaya.

Mahujaji wa Kihispania kutoka sehemu mbali mbali za dunia, kuanzia tarehe11 hadi tarehe 18 Agosti 2013 wanashiriki katika hija ya imani kwenye Madhabahu ya Bikira Maria wa Fatima. Kuna idadi kubwa ya wananchi wa Hispania ambao wamehama au kuikimbia nchi yao kutokana na athari za myumbo wa uchumi kimataifa. Hili ni kundi ambalo linahitaji kupatiwa msaada na huduma za kichungaji huko liliko!

Hii pia ni changamoto kwa waamini na wananchi wa Hispania katika ujumla wao, kuonesha moyo na mshikamano wa dhati kwa wakimbizi na wahamiaji kutoka sehemu mbali mbali za dunia; watu wanaotaka kusalimisha maisha yao kutokana na vita, kinzani na hali ngumu ya maisha.







All the contents on this site are copyrighted ©.