Jeshi la Polisi Uganda lasikitishwa na wezi wanaomwibia hata Mungu!
Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi nchini Uganda Kale Kayihura amesema amepokea
taarifa kutoka Jeshi la Polisi mjini Vatican ikimwomba kufanya uchunguzi wa kina kwa
watu wanaotuhumiwa kuiba fedha kutoka Benki ya Vatican na kuziwekeza nchini Uganda.
Jenerali Kayihura ameyasema hayo hivi karibuni alipokuwa anafungua mkutano
wa siku tatu wa wakuu wa Jeshi la Polisi kutoka Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika,
mkutano ambao umezishirikisha nchi 25.
Anasema, inasikitisha kuona watu wanamwibia
Mwenyezi Mungu? Vatican kwa sasa inaendelea kuboresha sheria na mikakati ya kupambana
na utakatishaji wa fedha haramu kama njia ya kusimamia misingi ya ukweli, uwazi, uadilifu
na uwajibikaji.
Wakati huo huo, habari kutoka Kampala Uganda zinasema kwamba,
Jeshi la Polisi nchini Uganda, linamshikilia Esther Nabasa kwa shutuma za kujipatia
kiasi cha Euro 287, 180, 000 sawa na shilingi Billioni 1 za Uganda.