Miaka 35 tangu alipofariki Mtumishi wa Mungu Paulo VI
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya Sala ya Malaika wa Bwana, Jumapili iliyopita
alikumbusha kwamba, tarehe 6 Agosti 2013, Kanisa litafanya kumbu kumbu ya miaka 35
tangu Mtumishi wa Mungu Papa Paulo wa VI alipofariki dunia, akiwa kwenye Ikulu Ndogo
ya Castel Gandolfo, nje kidogo ya mji wa Vatican.
Askofu Francesco Beschi wa
Jimbo Katoliki Bergamo, Italia anatarajiwa kuongoza Ibada ya Misa Takatifu kwenye
Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican majira ya jioni. Sr. Gisela Upendo Msuya
anatujuza kwa ufupi historia na mchango wa Mtumishi wa Mungu Papa Paulo wa VI.