Wafanyakazi wa sekta ya afya Kenya kulipwa kwa wakati!
Waziri wa Afya nchini Kenya, James Macharia amesema kwamba wauguzi watalipwa mishahara
yao kama ilivyopangwa ili kuzuia mgomo wa madaktari. Waziri amesema kwamba serikali
inajali maslahi ya wafanyakazi wa sekta ya afya kwani bila kufanya hivyo watu wengi
wanaweza kuathirika na madaktari hao hawatakuwa na uwezo mzuri wa kuwauguza wagonjwa.
Madaktari nchini Kenya walitishia kugoma ifikapo tarehe 4, Agosti 2013 ikiwa
serikali haitawapatia mishahara yao ya mwezi Julai. Kawaida mishahara hiyo hulipwa
kila tarehe 25 ya mwezi. Kupitia chama chao cha madaktari na wauguzi wa meno, wafanyakazi
hao wamesema hawaelewi ni kwa nini mishahara yao inacheleweshwa na Serikali.