Mama Kanisa anapoadhimisha Kumbu kumbu ya Mtakatifu Inyasi wa Loyola, Mwanzilishi
wa Shirika la Wayesuit, Baba Mtakatifu Francisko anawaalika vijana kujishikamanisha
katika maisha yao na Kristo pamoja na Injili, kwa kutoa sadaka mambo mengine yote
yawe ni kwa ajili ya matendo makuu ya Mungu. Huu ni ujumbe wa Baba Mtakatifu kwa ajili
ya watumiaji wa mitandao ya kijamii.
Baba Mtakatifu Francisko bado mawazo
yake yako nchini Brazil katika Maadhimisho ya Siku ya 28 ya Vijana Duniani kwa Mwaka
2013.