2013-07-29 12:05:05

Vatican na Italia kuendelea kushirikiana katika mapambano dhidi ya utakatishaji wa fedha haramu!


Mamlaka ya Habari za Fedha Vatican (AIF) tarehe 26 Julai 2013, imetiliana sahihi mkataba wa makubaliano na Mamlaka ya Habari za Fedha Italia (UIF) kutoka Benki kuu ya Italia. Kardinali Attilio Nicora, Rais wa AIF ameweka sahihi kwa niaba ya Vatican na kwa upande wa Italia, sahihi imewekwa na Dr. Claudio Clemente, mkurugenzi mkuu wa UIF.

Makubaliano haya ni jitihada za Vatican kwa kushirikiana na Serikali ya Italia kuongeza nguvu katika kupambana na utakatishaji wa fedha chafu katika nchi hizi mbili. Makubaliano haya yanatoa fursa kwa Serikali ya Italia na Vatican kushirikishana habari kuhusu fedha pamoja na kutunza siri. Vatican inaendelea kuimarisha juhudi zake za kupambana na utakatishaji wa fedha chafu pamoja na kugharimia vitendo vya kigaidi.

Kitengo cha kupambana na utakatishaji wa fedha chafu mjini Vatican kiliundwa hapo tarehe 30 Desemba 2010.







All the contents on this site are copyrighted ©.