Papa atuma salam za rambi rambi kutokana na kifo cha Kardinali Tonini
Baba Mtakatifu Francisko amepokea kwa masikitiko makubwa habari za kifo cha Kardinali
Ersilio Tonini, Askofu mkuu mstaafu wa Jimbo kuu la Ravenna- Cervia. Anapenda kuwahakikishia
wote wanaoomboleza msiba huu mkubwa uwepo wake kwa njia ya sala na sadaka kwa kumpoteza
mchungaji mchapakazi na mkarimu, aliyejipambanua kutokana na utume wake katika medani
mbali mbali za maisha na utume wa Kanisa.
Ni kiongozi aliyemtangaza Kristo
kwa watu wote huku akitumia lugha nyepesi pamoja na kuonesha ushuhuda wa maisha kwa
watu wa nyakati hizi. Ujumbe wa Baba Mtakatifu umeandikwa kwa niaba yake na Kardinali
Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican kwenda kwa Askofu mkuu Lorenzo Ghizzoni wa
Jimbo kuu la Ravenna. Baba Mtakatifu anawapatia baraka zake za kitume, wote wanao
omboleza msiba huu.