2013-07-25 11:41:24

Papa aguswa na ajali ya treni huko Compostela!


Baba Mtakatifu Francisko anaungana na ndugu, jamaa na wote waliopatwa na maafa kutokana na ajali ya treni iliyotokea huko Santiago de Compostella, Hispania, siku ya Jumatano, tarehe 24 Julai 2013 na kusababisha watu 77 kufariki dunia na wengine 140 kupata majeraha makubwa.

Hayo yamesemwa na Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa vatican alipokuwa anazungumza na jopo la waandishi wa habari lililoko kwenye msafara wa Baba Mtakatifu Francisko nchini Brazil. Baba Mtakatifu ameonesha nia ya kurudi tena nchini Brazil kunako mwaka 2017 wakati wa Jubilee ya miaka 300 tangu Sanam ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili ilipoibuliwa kutoka katika mto Paraiba.

Na Mwaka 2017, Madhabahu ya Fatima yatakuwa yanafanya Jubilee ya Miaka 100, itakuwa ni fursa kwa Baba Mtakatifu kutembelea maeneo haya.

Baba Mtakatifu wakati wa chakula cha mchana kwenye Seminari ya Kristo Mchungaji mwema, alipata fursa ya kusalimiana na Jumuiya pamoja na wafanyakazi; amewashukuru na kuwapongeza wapishi kwa kazi kubwa waliyoifanya na wengi wao wamefanikiwa kupata picha ya kumbu kumbu kwani hapa kulikuwa hakuna haraka anasema Padre Lombardi. Baba Mtakatifu ametumia muda wake wa mapumziko kwa ajili ya kusalimiana na kuzungumza na watu mbali mbali waliokuwepo Seminarini hapo.







All the contents on this site are copyrighted ©.