2013-07-24 08:51:56

Yesu ana matumaini na vijana!


Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya kuwasili nchini Brazil na kupata mapokezi makubwa, Jumanne alipumzika kidogo, huku akikusanya nguvu tayari kuanza pilika pilika pilika za Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2013. Askofu mkuu Oran Joao Tempesta wa Jimbo kuu la Rio de Janeiro, ndiye aliyeongoza Ibada ya Misa Takatifu kwa ajioli ya ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku ya 28 ya Vijana Duniani.

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa vijana wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho haya anawaambia kwamba, Yesu Kristo ana matumaini makubwa na vijana na anapenda kuwakabidhi utume wake akisema, basi enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa ni wanafunzi.

Wakati huu kuna Maaskofu 250 kutoka sehemu mbali mbali za dunia wanaoendesha Katekesi ya kina kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Vijana: Mada kuu zinazoongoza Katekesi hizi ni: "kiu ya matumaini, kiu ya Mungu"; "Jinsi ya kuwa mfuasi wa Yesu"; Iweni Wamissionari, nendeni". Katekesi hizi zinaendeshwa katika maeneo zaidi ya 300 yaliyotawanyika mjini Rio de Janeiro.







All the contents on this site are copyrighted ©.